Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya
nje, ulinzi na usalama wakimsikiliza kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara (hayupo
kwenye picha) akizungumza wakati wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya
ulinzi na usalama ya Mkoa katika kikao kilichofanyika Machi 19, 2018 katika Ofisi ya Mkuu
wa Mkoa.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge
ya Mambo ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Salum Rehani akizungumza jambo wakati
wa kupokea na kujadili taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa katika
kikao kilichofanyika Machi 19, 2018 ofisini kwake Mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo
ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na afisa
uhamiaji Mkoa wa Mtwara, James Mwanjotile (kulia) wakati kamati hiyo ilipoenda
kukagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara 19 Machi, 2018
Mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo
ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (kulia) akipokelewa na katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto)
wakati kamati hiyo ilipoenda kukagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara Machi 19, 2018 Mkoani Mtwara.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo
ya nje, ulinzi na usalama, Mhe. Mussa Zungu (katikati) akisisitiza jambo pale
kamati hiyo ilipokuwa inakagua ujenzi wa ofisi za uhamiaji Mkoa wa Mtwara Machi 19, 2018 Mkoani Mtwara.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)


0 Comments