Kijana akiwa kihwa chini miguu juu, tena hewani wakati akicheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
Wasani wa kikundi cha sanaa cha Vijana wa Smangila wakionyesha uhodari wa kucheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
Wanawake wajasriamali wa Kata ya Somangila wakijimwayamwaya kucheza muziki kufurahia uzinduzi wa Jukwaa.
Diwani wa Kata ya Somangila Wilayani Kigamboni, Francis Chichi (kulia) akionyesha umahiri wa kusakata muziki pamoja na Kinamama wakati wa Uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata hiyo,
Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akiungana na Wanawake wajasiriamali kusakata muziki wakati wa sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila
Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akicheza ngoma na msanii wa kikundi cha Vijana wa Somangila wakati wa Sherehe hizo za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila
Wanawake wa vikundi vya Wajasiriamali wakiandamana kutoka kwenye Ofisi yao kwenda kwenye uwanja wa Dege, kwenye Uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila Wilayani Kigamboni, Dar es Salaam,
Mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila, Kigamboni Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali (kulia) akiwa na baadhi ya Viongozi wa Jukwaa hilo wakati wakipokea maandamano ya Wanawake Wajasiriliamali kwenye uzinduzi wa Jukwaa hilo
Viongozi wa Vikundi mbalimbali vya Wanawake Wajasiriamali na Jukwaa la Wanawake wakiwa tayari kupokea maandamano ya wanawake Wajasiriamali. Kushoto ni Mgeni Rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM angel Akilimali akipunga mikono
Viongozi wakimwayamwaya kupokea maandamano hayo
Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali akisoma moja ya mabango waliyokuwa nayo Wanawake Wajasiliamali walipowasili Uwanjani kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila.
Mwanamke Mjasiriamali wa kutengeneza vifaa vya ujenzi Amina Zakumera (kushoto) akimpatia maelezo ya utaalam wake Mgeni Rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali (Wapili kulia) alipokuwa akikagua bidhaa za Wanawake wajasiriamali wakati wa uzinduzi wa jukwaa la Wanawake wa Kata ya somangila, Kigamboni,
Angel Akilimali akipata maelezo kuhusu bidhaa za mwanamke Mjarismali Winifrida Jafari (kushoto) wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somanga, Kigamboni leo. Wapili kushoto ni Mjasiriamali Joha Amour wa Joha Fashion.
Angel Akilimali akitazama mkeka uliotengenezwa na Mwanamke Mjasiriamali Jawa Maulidi (kushoto)
Angel Akilimali (kushoto) akimuuliza Mwanamke Mjasiriamali jinsi anavyotengeneza bidhaa zake.
Angel Akilimali na Diwani Chichi wakinywa togwa kwenye banda la maonyesho la Mwanamke Mjasiriamali, wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni.
Mtendaji wa Kata ya Somangila Munna Msafiri akitambulisha viongozi wa vikundi mbalimbali na Jukwaa la wanawake kutoka maeneo mbalimbali
Viongozi wa Majukwaa ya Wanawake kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Kigamboni wakitambulishwa
Diwani wa Kata ya Somangila Ndugu Chichi akifanya harambee ya uchangiaji wa fedha kutunisha mfuko wa Jukwaa la wanawake katika kata yake.
Mkuu wa Polisi Kata ya Somangila Mwakila Chile akizungumza baada ya kutambulishwa na Diwani Chichi
Mgeni rasmi katika Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya somangila Kigamboni Angel Akilimali akifurahia vijana walivyokuwa wakionyesha uhodari wa kucheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
Mgeni rasmi katika sherehe za Uzinduzi wa Jukwaa la wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni, Angel Akilimali akinadi kiatu alipoendesha mnada wa vitu mbalimbali vya wanawake wajasriamali wakati wa sherehe hizo
Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akikitazama kwa makini kiatu hicho baada ya kukubali kukinunua kwa sh 50,000
Angel Akilimali akipongezwa na MC katika sherehe hizo
Angel Akilimali akiwa na mtunza Fedha wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Kigamboni Pili Doto mwishoni wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake kata ya Somangila
Angel Akilimali (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa New Life Queen Bahati mwishoni mwa sherehe hizo
Angel Akilimali akiwa na baadhi ya Wanawake wajasiriamali
Mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la wanawake Kata ya Somangila, Kigamboni Dar es Salaam, Angel Akilimali akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Jukwaa hilo katika kata mbalimbali za Kigamboni na Viongozi wa vikundi vya Wanawake wajasiriamali wa kata hiyo baada ya uzinduz
Angel Akilimali akihutubia Wakati wa Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni
Angel Akilimali akihutubia Wakati wa Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
Na Bashir
Nkoromo, Kigamboni
Wanawake wajasiariliamali wametakiwa kutengeneza au kuuza bidhaa zenya
ubora wa viwango vinavokubalika ili kuvutia wateja kununua bidhaa zao na
kuongeza masoko ndani na nje ya Nchi.
Hayo yamesemwa leo na
Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali ambaye alikuwa mgeni rasmi katika
uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila, Manispaa ya Kigamboni jijini
Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huo
uliofanyika Uwanja wa Dege katika Kata hiyo Angela alisema mbali na na
bidhaa bora kuhamasisha wanunuzi na kuongeza masoko ndani na nje ya Nchi
boa bidhaa hizo zinaweza kumudu ushindani katika soko.
Alivishauri vikundi vya
Wanawake wajasiriamali kwenda kuomba mikopo kwenye Benki ya Wanawake Tanzania
ambayo alisema ni benki yenye mikopo ya riba nafuu.
Uzinduzi wa Jukwaa hilo ni
sehemu ya shamrashamra za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo
yatafanyika mapema mwezi huu.































0 Comments