Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Aggrey Mwanri akisisitiza jambo wakati akifungua kongamano la siku moja
la wadau wa afya lilokuwa likiwaelimisha juu ya maandalizi ya chanjo ya
kuwakinga wasichana na saratani ya shingo ya kizazi jana mjini Tabora. Chanjo
hiyo inazinduliwa tarehe 23 Mwezi huu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt . Gunini Kamba akitoa maelezo juu ya uendeshaji wa chanjo ya kuwakinga wasichana dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi wakati wa kongamano la wadau wa afya jana mjini Tabora. Chanjo hiyo inazinduliwa tarehe 23 Mwezi huu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt . Gunini Kamba akitoa maelezo juu ya uendeshaji wa chanjo ya kuwakinga wasichana dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi wakati wa kongamano la wadau wa afya jana mjini Tabora. Chanjo hiyo inazinduliwa tarehe 23 Mwezi huu.
NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
ZAIDI wasichana elfu 30 wenye umri wa miaka ( 14 )
wanatarajiwa kupata chanjo ya kinga ya Saratani ya mlango wa kizazi mkoani
Tabora kuanzi wiki ijayo.
Kauli
hiyo ilitolewa jana mjini hapa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora(RMO) Gunin Patrick
Kamba wakati wa kongamano la siku moja na wadau wa afya.
Alisema
kuwa chanjo hiyo maalumu kwa watoto wa kike wenye umri wa miaka 14 itazinduliwa
Aprili 23 mwaka huu katika Manispaa ya Tabora na Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya
maeneo mengine mkoani humo.
Dkt.
Gunini alisema kuwa serikali imechukua hatua za makusudi kutoa chanjo hiyo ya
saratani ya mlango wa kizazi kwa watoto wa kike kwani uchunguzi umebaini kwamba
kundi hili ndilo lenye hatari ya kupata maambukizi kwa urahisi.
Mganga
Mkuu huyo wa mkoa aliongeza kuwa lengo la Serikali ni kuwapatia chanjo watoto
wa kike wa kuanzia miaka tisa lakini kwa kuanzia watakaohusika ni wenye miaka
14 ikiwa ni njia mojawapo ya kupunguza vifo vya akinamama vinavyosababishwa na
saratani.
Aliongeza
kuwa kinachochangia kuwepo kwa tatizo hilo kwa wingi ni pamoja na akina mama
wengi kutofika kwenye vituo vya afya kupima.
Awali
akifungua kongamano hilo Mkuu wa Mkoa huo Aggrey Mwanri alisema Serikali
haitasita kuwachukulia hatua wale wote watakaokwamisha kwa namna moja ama
nyingine utekelzaji wa zoezi hilo.
Mwanri
alisema kuna baadhi ya watu kwa makusudi
ama kwa kutokujaa wanaopotosha wakidai kuwa chanjo hizi zinazotolewa kwa watoto
kwamba ni kinga ya uzazi zitawafanya wasizae kumbe sio kweli na kuwaweka katika
hatari.
Aidha aliwatadharisha
watumishi wote wanaosimamia zoezi la mkubwa kwani haitasita kuchukua hatua kwa
yeyote atakayejaribu kwa namna moja au nyingine
kukwamisha.
Alisema
kuwa Chanjo hiyo inagharama kubwa wanaopotosha wanakusudia kuisababishia hasara
Serikali na kuwaweka wasichana katika hatari na hivyo watachukuliwa hatua
wakibainika.
Mkuu
huyo wa Mkoa alitoa wito kwa wazazi kuwahimiza mabinti zao kujitokeza kwa wingi
ili kupata chanjo hiyo kwa sababu kinga ni bora kulikoa tiba ili hatimaye
wasalimike na madhara yatokanayo na Saratani ya shingo ya uzazi.
Chanjo hiyo ya kukinga saratani ya
mlango wa kizazi (HPV Vaccine), ilizinduliwa hivi karibuni na Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya
Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.


0 Comments