Ndugu
jamaa na marafiki waliungana pamoja na jamii ya wafanyabiashara kutoka nchini
China kutoa salamu zao za mwisho wakati wakimuaga Bi Lin Xiuling (45) mke wa
mfanyabiashara raia wa China anayefanya shughuli zake kariakoo jijini Dar es
salaam.
Bi Lin Xiuling aliuwawa nyumbani kwake
Karikaoo na watu wanaosadikika kuwa ni majambazi mnamo Marchi 13, 2018 majira ya asubuhi.
Majonzi vilio na huzuni zilitawala kwa waombolezaji pale katika viwanja vya Mnazi mmoja Dar es salaam ambapo watu waliungana pamoja katika ibada ya kutoa heshima zao za mwisho na kumuaga Bi Lin.
Marehemu alikuwa ni mfanyabiashara kutoka katika jimbo la Fu Jian nchini China, alikuja Tanzania mnamo tarehe 8 March ili kuungana na mumewe katika kufanya biashara. Bi Lin ameacha mume na familia ya watoto wawili.
Akizungumza
mwenyekiti wa jumuiya ya wachina wanaofanya biashara kariakoo Bwana Xu Huo Pao,
alisema Lin alitoka China kuja Tanzania kufanya biashara ya kuuza mapazia na
vyandarua ambapo ndoto yake ilikatishwa ndani ya siku 24 tu tangu alipowasili
nchini hapa.
Katika
Ibada ya kuaga mwili wa marehemu Lin Xiuling Mkuu wa wilaya ya Ilala Sofia
Mjema ameliomba jeshi la polisi kuharakisha uchunguzi wa mauaji hayo na
kuhakikisha waliohusika wanapatikana.
“Jitihada zimefanyika na hadi sasa amepatikana
mtu mmoja kati ya wawili wanaosadikika kufanya mauaji hayo” alisema Mjema.
Pia amewaomba wafanyabiashara kutoka China na
nchi mbalimbali kuwa waangalifu katika biashara zao na kujiwekea ulinzi wa
kutosha katika utunzaji wa mali zao hasa fedha nyingi wawe na utaratibu
wa kuhifadhi benki pia amewashauri kuomba jeshi la polisi kuwapa ulinzi katika
kusafirisha mali hizo.
Sofia Mjema aliwaambia wafanyabiashara hao kutoka
China kuwa serikali itahakikisha kuwa wanafanya biashara zao kwa utulivu na
Amani.


0 Comments