Mwenyekiti wa Baraza la wataalamu wa maabara Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto, Viola Msangi akifungua kikao kifupi cha kutoa taarifa huduma na majukumu za maabara kwa watanzania (kushoto) Mkurugenzi
Msaidizi wa Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa, Dkt Charles Massambu, kilichofanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam Mei 22, 2018.
Msajili wa Baraza la wataalamu wa maabara, Theophil Malibiche akielezea muundo wa Baraza hilo na majukumu yake wakati wa kikao cha kutoa taarifa kuhusiana utoaji huduma za maabara kwa watanzania kilichofanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam Mei 22, 2018.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa kutoka Wizara ya
Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Charles Massambu akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za wizara hiyo Jijini Dar es Salaam Mei 22, 2018 wakati wa kikao cha Baraza
la wataalamu wa Maabara kuhusiana na huduma za zinazotolewa na Baraza hilo.
Msajili wa Baraza la wataalamu wa maabara, Theophil Malibiche akielezea muundo wa Baraza hilo na majukumu yake wakati wa kikao cha kutoa taarifa kuhusiana utoaji huduma za maabara kwa watanzania.
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la wataalamu wa maabara, Dr. Edda akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho.
Mkuu wa Huduma za Maabara Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto, Dickson Majige (kushoto) pamoja na wajumbe wataamu wa maabara wakiwa katika kikao kifupi cha kutoa taarifa huduma na majukumu za maabara kwa watanzania
Seemu ya waandishi wa habari wakiwa katika kikao hicho.
Picha na Philemon Solomon
Mkurugenzi Msaidizi Huduma ya uchunguzi na magonjwa kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Charles Massambu ( kushoto) akisisitiza juu ya umuhimu wakujisajili katika huduma za maabara (kulia) Mwenyekiti wa Baraza la wataalamu wa maabara, Viola Msangi.
..........................
Na Happy Daudi-Mtazamo News
Baraza la Wataalam wa Maabara nchini limewataka watoa huduma za kimaabara kwa wananchi kuhakikisha wanakuwa
na vibali kwani kinyume na hapo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao kwa
mujibu wa wa sheria.
Mkurugenzi
Msaidizi Huduma ya uchunguzi na magonjwa kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na
Watoto Dk. Charles Massambu amesema sheria itachukua
mkondo wake kwa wale wanaotoa huduma kwa wananchi za kimaabara bila vibali vya kusajiliwa.
Ameyasema hayo wakati wa kikao cha waandishi
wa habari kutoa taarifa kuhusu majukumu na kazi zinazotolewa na baraza hilo kilichofanyika
katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam Mei 22, 2018.
"Hakuna
mtoa huduma atakaetoa huduma za maabara bila kusajiliwa tukibaini tutachukua
hatua za kisheria," amesema Dk. Massambu.
Massambu
amesema baraza linatambua uwezo na utaalamu katika kuelimisha jamii ya
watanzania kuhusu majukumu katika kuwahudumia na changamoto za majibu ya vipimo
kutofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine Wizara imechukua hatua ya uhakiki
wa ubora wa vipimo.
"Tanzania
kuna maabara 33 ambazo ni nyota moja mpaka nne,nyingine nane zilizo na hadhi ya
kimataifa ambapo vipimo vyake huwa ni sawa na vya nchi nyingine za nje.
Akifafanua
Vigezo vya maabara amesema katika ngazi
ya taifa na kanda vibali vimetolewa na Shirika la Afya Duniani ambapo waliamua
kutoa nyota za viwango vya ubora hatua kwa hatua.
Ameviomba
vyombo vya habari kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na madhara ya matumizi ya
maabara ambazo hazisajiliwa na baraza hilo ili kuwasaidia wananchi kupata
vipimo sahihi pamoja na kuwapunguzia gharama za matibabu.
Kwa upande
wa Msajili wa Baraza hilo Theophil Malibiche amesema kisheria zipo gharama
kidogo zinazoendana na usajili wa wataalamu wa maabara ambazo zimegawanyika
katika usajili wa awali na wa kudumu kwa kiwango tofauti cha elimu ada ya kila
ambayo kila mwaka.









0 Comments