Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza
na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI wakati akifunga
mkutano wa siku moja siku moja uliofanyika mjini hapo ulio chini ya Mradi wa SAUTI unalenga kuhakikisha hakutakuwepo na maambukizi mapya ifikapo mwaka 2030.
Mkuu wa Wilaya Quuen Mlozi akitoa maoni yake jana mjini Tabora wakati wakati wa mkutano wa siku moja wa wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI chini ya
Mradi wa SAUTI unalenga kuhakikisha hakutakuwepo na maambukizi mapya ifikapo mwaka 2030.
Mkuu
wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula (kulia mstari wa mbele) , Mkuu wa
Wilaya ya Abel Busala (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres
Magiri (kushoto) na viongozi wengine walionyuma yao wakifuatilia hotuba
ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo katika picha) wakati wa kufungua
mkutano wa siku moja wa wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI
Mkuu wa Wilaya
ya Urambo Angelina Kwingwa(kulia mstari wa mbele) na Mkuu wa Wilaya ya
Igunga John Mwaipopo(kushoto mstari wa mbele) na viongozi wengine
walionyuma yao wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo
katika picha) wakati wa kufungua mkutano wa siku moja wa wadau wa
mapambano dhidi ya UKIMWI
Baadhi ya washiri wa mkutano wa siku moja
wakifuatilia
hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo katika picha) wakati wa
kufungua mkutano huo wa wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
Baadhi ya Wenyeviti wa Halmashauri mbalimbali mkoani Tabora wakifuatilia
hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo katika picha) wakati wa
kufungua mkutano huo wa wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI ulifanyika
jana. Walio nyuma yao ni wajumbe wa mkutano huo.
Meneja Mwandamizi
Utekelezaji wa Mradi wa SAUTI kutoka Shirika la Jhpiego Nelson
Rutabanzibwa akizungumza jana mjini Tabora na waandishi wa habari juu ya
malengo ya mradi huo ambao unalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka
2020 watu wote waliopata ushauri nasaha na kupima na kugundulika wana
maambukizi wawe wanajua hali zao na wale wanatumia dawa za kufubaza VVU.
NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
6 May 2018
MKUU wa Mkoa wa Tabora Aggrey
Mwanri amewaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halamashauri zote kuhakikisha
wanatenga maeneo mengi kwa ajili ya uanzishaji wa vituo ambavyo wananchi
watakwenda kupata ushauri nasaha na kupima kwa hiari ikiwa ni sehemu ya kujinga
na UKIMWI.
Alitoa wito huo jana mjini
Tabora wakati akizungumza na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI
kwenye mkutano wa siku moja.
Alisema hatua hiyo ni muhimu kwa ajili ya kutoa
elimu katika maeneo mengine
yenye mkusanyiko wa watu wengi juu ya kujikinga
kwa wale ambao bado hawajapata maambukizi na wale ambayo tayari wapate dawa za
kufubaza virusi(ARVs).
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alisema utafiti ubaini kuna mwako mdogo kwa wanaume
kupima na kutumia dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi (ARVs) na kutoa
wito kwa wanaume kujenga tabia kuongozana na wake zao
katika kwenda kupata ushauri nasaha na kupima VVU.
Alisisitiza woga wa baadhi ya wanaume unaweza kikwazo
katika mapambano dhidi ya Ukimwi katika jamii.
“Baadhi ya wanaume wengi wanaogopa kwenda kupima…mara
nyingi wanasubiri majibu ya wake zao wakiona amepata majibu kuwa hana
maambukizo naye anaamini kwamba yuko salama , jambo ambalo linaweza lisiwe
kweli…ni vema elimu itolewe ili wenza waende kupima wote” alisema Mwanri.
Naye Meneja Mwandamizi Utekelezaji wa Mradi wa SAUTI kutoka Shirika la Jhpiego
Nelson Rutabanzibwa alisema mradi huo unalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka
2020 watu wote waliopata ushauri nasaha na kupima na kugundulika wana
maambukizi asilimia 90 wawe wanajua hali zao na wale wanatumia dawa za kufubaza
VVU , hatua itakayosaidia kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vinavyosababisha
UKIMWI.
Rutabanzibwa aliongeza kuwa mradi
huu unalenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030 kusiwepo na vifo vinavyotokana
na Virusi vya Ukimwi, unyanyapa usiwepo na hakuna maambukizi mapya.
Alisema mradi huu unalenga
kusaidi juhudi za Serikali katika mwitikio dhidi ya VVU hasa kwa makundi
maalumu yaliyo kwenye hatari ya kupata maambukizi ama kuambukizwa kama wale
wanafanya biashara ya mapenzi.
Kwa upande
wa Mkuu wa Wilaya Tabora Queen Mlozi aliwawataka wadu mbalimbali kuendelea
kutoa elimu zaidi kwa wananchi ili wajitokeze kwa wingi katika maeneo yao kupima
na kujua afya zao.
Mradi
wa SAUTI unaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Ofisi ya Rais Tawala za
Mikoa na Serikali za MItaa(TAMISEMI) na
kutekelezwa na Shirika
la jhpiego kwa kushirikiana na mashirika
ya Engender Heath, Pact Tanzania na NIMR
tawi la Mwanza chini ya ufadhili wa Mfuko
wa dharula wa Rais wa Marekani wa kupamana na UKIMWI kupitia Shirika la
Maendeleo la Kimataifa la Watu wa Marekani (USAID) .
Mradi huo ambao ni miaka mitano unatekelezwa katika mikoa 14 na Halmashauri 51 ya Tanzania Bara.







0 Comments