Random Posts

Jumuia ya Kihindu Tanzania (BAPS) Imetoa Kiasi cha Shilingi milioni 68 Kulipia Matibabu ya Upasuaji wa moyo kwa watoto

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na kaimu kiongozi wa Jumuia ya Kihindu  Duniani (BAPS) Mtukufu Bhaktipriyadas  Swami  pamoja na viongozi wengine wa jumuia hiyo wa hapa nchini wakati kiongozi huyo alipotembelea Tanzania  hivi karibuni. BAPS imetoa kiasi cha shilingi milioni 68 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto 30.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akisalimiana na  kaimu kiongozi wa Jumuia ya Kihindu  Duniani (BAPS) Mtukufu Bhaktipriyadas  Swami  alipotembelea Tanzania  hivi karibuni. BAPS imetoa kiasi cha shilingi milioni 68 fedha ambazo zitatumika kwaajili ya kulipia gharama za  upasuaji wa moyo kwa watoto 30.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi na  Viongozi wa Jumuia ya Kihindu  (BAPS) wakijadili jambo wakati  Kaimu kiongozi wa Dunia wa Jumuia hiyo Mtukufu Bhaktipriyadas  Swami  alipotembelea Tanzania  hivi karibuni. BAPS imetoa kiasi cha shilingi milioni 68 fedha ambazo zitatumika kwaajili ya kulipia gharama za  upasuaji wa moyo kwa watoto 30.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na  kaimu kiongozi wa Jumuia ya Kihindu  Duniani (BAPS) Mtukufu Bhaktipriyadas  Swami  alipotembelea Tanzania  hivi karibuni. Tangu mwaka 2016 BAPS wamekuwa wakitoa fedha kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto ambapo hadi sasa jumla ya watoto 290 wameshafanyiwa upasuaji.
Kaimu kiongozi wa Jumuia ya Kihindu  Duniani (BAPS) Mtukufu Bhaktipriyadas  Swami  akimpa zawadi  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati kiongozi huyo alipotembelea nchini  hivi karibuni. Tangu mwaka 2016 BAPS wamekuwa wakitoa fedha kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto ambapo hadi sasa jumla ya watoto 290 wameshafanyiwa upasuaji na hali zao zinaendelea vizuri.


Picha na JKCI

Na Mwandishi  Maalum,

Jumuia ya Kihindu Tanzania (BAPS) imetoa kiasi cha shilingi milioni 68 fedha ambazo ziatumika kwaajili ya kulipia gharama za matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto wenye matatizo hayo  hapa nchini.

Fedha hizo ambazo   zitatumika kwaajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 30 wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) zimetolewa hivi karibuni na kaimu kiongozi wa Dunia wa jumuia hiyo.

Akizungumza kuhusu msaada huo Kaimu kiongozi wa Jumuia ya Kihindu Duniani Mtukutu Bhaktipriyadas  Swami alisema wametoa fedha hizo kwa ajili ya kusaidia  jamii yenye uhitaji hasa watoto wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi alishukuru kwa msaada huo na kusema kuwa fedha zilizotolewa zitatumika kwa walengwa ambao ni watoto wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo.

Prof. Janabi alisema kuwa Taasisi hiyo imekuwa na  uhusiano mzuri na Jumuia ya BAPS ambao kila mwaka wamekuwa wakichangia fedha kwaajili ya matibabu ya moyo kwa watoto ambao baada ya matibabu wamepona na wengine wamerudi shuleni kuendelea  na masomo yao.

Tangu mwaka 2016 BAPS wamekuwa wakitoa fedha kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto ambapo hadi sasa jumla ya watoto 290 wameshafanyiwa upasuaji.

Post a Comment

0 Comments