Mjumbe wa baraza Kuu la umoja wa wanawake Tanzania (UWT) mkoani Pwani
,Nancy Mutalemwa akizungumza katika mafunzo ya kujengewa uwezo kwa
Jukwaa hilo ,Kibaha Mjini yaliyoandaliwa na kampuni ya Ae General
Business Co Ltd.
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Baadhi ya akinamama wajasiriamali mjini Kibaha wakisikiliza jambo,wakati
walipokuwa wakipatiwa mafunzo ya kujengewa uwezo kwa Jukwaa hilo
,Kibaha Mjini yaliyoandaliwa na kampuni ya Ae General Business Co
Ltd.
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Mkurugenzi wa Ae General Business Co Ltd Alexander Malya,(Wa Kushoto
aliyesimama) akimsikiliza Katibu Wa jukwaa la uwezeshaji Wanawake
Mkoani Pwani Elina Mgonja akielezea jambo katika mafunzo ya kujengewa
uwezo kwa Jukwaa hilo ,Kibaha Mjini yaliyoandaliwa na kampuni ya Ae
General Business Co Ltd.
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha
KATIBU wa jukwaa
la uwezeshaji wanawake mkoani Pwani ,Elina Mgonja ,amewataka wanawake
kuthubutu kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili kuunga mkono juhudi za
Rais Dk John Magufuli ya kufikia uchumi wa kati.
Aidha
amewaasa wanawake kuacha kukata tamaa kwani wana nafasi kubwa ya kukuza
uchumi na kuleta mapinduzi ya kimaendeleo kupitia shughuli zao za
ujasiriamali .
Akizungumza katika mafunzo ya kujengewa
uwezo kwa Jukwaa la Uwezeshaji la Wanawake ,Kibaha Mjini yaliyoandaliwa
na kampuni ya Ae General Business Co Ltd, alisema mwanamke akijiamini
anaweza .
Elina alieleza kuwa changamoto kubwa
inayokabili wanawake wajasiriamali ni ukosefu wa mikopo yenye riba
nafuu, elimu ya ujasiriamali kwa ajili ya kutengeneza na kuboresha
bidhaa zao .
Alisema licha ya vikwazo hivyo lakini haina
budi kukimbilia fursa nyingine zilizopo ikiwemo kuunda vikundi ili
kuwezeshwa kirahisi kupitia halmashauri na wadau mbalimbali.
"Wanawake
tukiamua tunaweza ,kuna kila sababu kuacha kukatishana tamaa ,kuwekeana
majungu hali inayosababisha kurudisha nyuma wenye nia "
"Nawaomba
wenye uwezo wa kuanzisha viwanda vidogo mthubutu kwani naamini mtaweza
ili kuongeza ajira na kuinua uchumi " alisema Elina .
Pamoja
na hayo Elina alisema ,suala la wazo nalo ni muhimu katika biashara
yoyote , bila kuwa na wazo ni ngumu kuwa na mafanikio hata kama mwanamke
atawezeshwa kifedha.
Nae mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja
wa Wanawake Tanzani (UWT) mkoa wa Pwani ,Nancy Mutalemwa ,alielezea
wanawake ni sehemu kubwa ya kukuza uchumi wa nchi kutokana na kuwa ni
wawajibikaji wakubwa na wamefanikiwa kubuni biashara ambazo zimewainua
kiuchumi.
Alisema kuwa kikubwa kinachotakiwa ni wao kuungana na kuanzisha viwanda vidogo kupitia vikundi vyao ambavyo wameviunda.
"Mna
nafasi kubwa ya kuinua uchumi wa nchi pia kupitia viwanda vilivyopo
hapa Pwani mnaweza kushiriki kukuza uchumi moja kwa moja au kuuza bidhaa
ambazo zitatumiwa na viwanda hivyo," alisema Nancy.
Kwa
upande wake ,mkurugenzi wa Ae General Business Co Ltd Alexander Malya
alieleza ili wanawake wafikie adhma hiyo ya uchumi wa kati wanapaswa
kubadilika kwa kuboresha bidhaa zao ili ziwe na ubora na viwango.
Malya
alisema ,moja ya mbinu za kuweza kuufikia uchumi wa kati ni wao kufanya
kazi kwa bidii na kujituma na kuachana na makundi ambayo hayawezi
kuwasaidia.




0 Comments