Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu akitoa salamu za Serikali mkoani Tabora mara baada ya kuhudhuria ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser.
Maaskofu na viongozi wa madhehebu mbalimbali walioalikwa kuhudhuria ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser(hayupo katika picha) wakifuatilia ibada hiyo jana mjini Tabora
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser akiwekwa wakfu wa kuwa Askofu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser akiwekwa wakfu wa kuwa Askofu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser akikabdiwa fimbo mara baada ya kuwekwa wakfu wa kuwa Askofu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu (katikati) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kushoto) wakati ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser(hayupo katika picha). Kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora Hassan Wakasubi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Robert Msalika (kushoto) mara baada ya kuwasili Mkoani Tabora kwa ajili ya kuhudhuria ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser(hayupo katika picha)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Angelina Kwingwa(kushoto) mara baada ya kuwasili Mkoani Tabora kwa ajili ya kuhudhuria ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati Askofu Dkt. Isaac Laiser(hayupo katika picha)
………………
NA TIGANYA VINCENT
TABORA
SERIKALI imesema haikatii kukoselewa na mtu au kikundi chochote isipokuwa inachosisitiza ni matumizi mazuri ya lugha wakati wa ukosoaji na sio kutumia lugha inachochea chuki na migawanyiko miomngoni mwa wananchi.
Kauli hiyo imetolewa leo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu kwenye ibada ya kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania , Dayosisi ya Magharibi Kati –Tabora.
Alisema Serikali haina dini lakini watu wake wana dini zao hivyo itaendelea kushirikiana na viongozi wa dini ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kutenda mema kwa ajili umoja wa nchini.
Makamu wa Rais alisema Serikali haitamvumilia mtu yoyote ambaye atataka kuwagawa Watanzania kwa misingi ya ukabili, udini na hata itikadi za kisiasa.
Aliwataka viongozi wa dini nchini kuendelea kuhubiri amani kila wakati na kusema kuwa kwa upande wa Serikali amani na usalama wa wananchi ndicho kipaumbele chake cha kwanza na hivyo itaendelea kuhakikisha Tanzania inabaki na umoja wake.
Naye Mkuu wa Kanisa la KKKT Askofu Dkt. Fredrick Shoo alisema Kanisa linaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano katika za kupigania haki mbalimbali za Watanzania.
Aliitaka Serikali kuwachukulia hatua wale wote ambao wanataka kulichonganisha Kanisa hilo na Serikali kwa tumia mitandao na vyombo mbalimbali kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Askofu Shoo alisema Kanisa litaendelea kutumia njia za kistarabu kuishauri Serikali na kama kukitokea tofauti watajadiliana na kumaliza mambo kistarabu na sio kama watu ambao wana nia mbaya wanavyochochea.
Kwa upande wa Askofu wa Kwanza wa Dayosisi ya Magharibi Kati –Tabora Askofu Dkt. Isaac Kissiri Laiser alisema Kanisa hilo lipo tayari katika kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa Viwanda mkoani Tabora ili kuelekea katika uchumi wa kati.
Katika sherehe hizo Makamu wa Rais aliichangtia Dayosisi hiyo milioni 3 kwa ajili ya kuongezea katika azma yao ya kujenga Kituo cha Afya.









0 Comments