KAMPUNI YA BIOSUSTAIN YAANZA MKAKATI WA ELIMU KILIMO CHA PAMBA SINGIDA - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, 30 September 2022

KAMPUNI YA BIOSUSTAIN YAANZA MKAKATI WA ELIMU KILIMO CHA PAMBA SINGIDA

Wakala wa Ununuzi wa Pamba wa Kampuni ya Biosustain Ltd inayojishughulisha na Kilimo cha Pamba mkoani Singida, Said Abdallah, akitoa taarifa wakati wa ufunguzi wa kongamano la msimu wa kilimo 2022/2023 wilayani Iramba lililofanyika Septemba 28, 2022.
 Balozi wa Pamba Nchini,  Aggrey Mwanri alitoa mafunzo ya kilimo cha zao hilo kwa wakulima.
 Balozi wa Pamba Nchini,  Aggrey Mwanri akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba Tanzania, James Shimbe akizungumza katika kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi akizungumza.
 Balozi wa Pamba Nchini,  Aggrey Mwanri akiwapa kiapo wakulima wa zao hilo ili wazingatie kanuni na sheria za kilimo bora cha pamba.
............................................................

Dotto Mwaibale na Philemon Mazalla, Singida

KAMPUNI ya Biosustain Ltd inayojishughulisha na kilimo cha pamba mkoani Singida imejipanga kutoa elimu kwa wakulima ili kuliendeleza zao hilo mkoani hapa.

Hayo yamebainishwa na Wakala wa ununuzi wa pamba wa kiwanda hicho Said Abdallah wakati akizungumza katika  ufunguzi wa kongamano la msimu wa kilimo 2022/2023 wilayani Iramba mkoani Singida lililofanyika Septemba 28, 2022.

“Kwa msimu huu wa kilimo kampuni yetu imejipanga kutoa elimu elekezi kwa wakulima ili waweze kulima na kuvuna kwa tija” alisema Abdallah.

Alisema kampuni hiyo ina uwezo wa kuchakata pamba tani 50,000 lakini kutokana na kuwa na msimu mbaya wamechakata tani 20,000 tu na kusababisha kuwa chini ya kiwango.

Alisema elimu hiyo wataitoa kwa kuzunguka kijiji hadi kijiji wakishirikiana  na Balozi wa Pamba Nchini, Aggyey Mwanri ambapo watatoa miundombinu wezeshi ya pikipiki na baiskeli ili kufanikisha jambo hilo.

Alisema kwa msimu uliopita walitoa baiskeli 20 na msimu huu wa 2022/2023 watatoa tena baiskeli zingine 22 kwa wakulima viongozi katika kila kijiji ambacho hakikuweza kufikiwa msimu uliopita.

Aidha Abdallah alisema watatoa pikipiki kwa maafisa ugani wa kampuni na pia watatoa mafuta kwa maafisa kilimo wa Serikali kwa ajili ya  vyombo vyao vya usafiri lengo likiwa kufanikisha kazi hiyo.

“Pamba ni zao lenye tija wakati wote inyeshe mvua, liwake jua itaota tu hivyo wito wangu kila mkulima na mwananchi mliopo hapa mlime walau kila mmoja ekari moja” alisema Abdallah.

Abdallah aliongeza kuwa msimu uliopita walivuna tani 700 lakini msimu huu wamevuna tani 861 na kuwa walisambaza mbegu tani 138 ambayo walitarajia kupata ekari 13,000 na kwa mavuno ya kiwango cha chini walitarajia kupata kilo milioni 4 lakini kwa bahati mbaya wamepata tani 800.

Katika ufunguzi wa kongamano hilo Balozi wa Pamba Nchini,  Aggrey Mwanri alitoa mafunzo ya kilimo cha zao hilo kwa wakulima ambapo alitumia nafasi hiyo kuipongeza kampuni hiyo kwa kuwa kinara wa uzalishaji wenye tija wa zao hilo mkoani Singida.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages