Subscribe Us

header ads

MABWAWA MATATU YA KUTIBU MAJITAKA KUJENGWA MANISPA SINGIDA, RC SERUKAMBA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI MKATABA

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba ( katikati waliosimama kushoto) pamoja na viongozi wengine wakishuhudia zoezi la  utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mabwawa matatu  ya kutibu majitaka baina ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA)  na mkandarasi M/S Perntels Company and Nangai Engineering and Contractors Co.(T) Ltd. 

Mkurugenzi Mtendaji wa SUWASA, Sebastian Warioba (kulia) wakibadilishana nyaraka baada ya kutiliana saini mkataba wa ujenzi wa mabwawa matatu  ya kutibu majitaka baina ya SUWASA na mkandarasi M/S Perntels Company and Nangai Engineering and Contractors Co.(T) Ltd.  (kushoto) Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Richard Magembe.
Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Richard Magembe (kulia) akielezea mchoro wa ramani ya  ujenzi wa mabwawa hayo yatakavyokuwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba.
Mkurugenzi Mtendaji wa SUWASA, Sebastian Warioba akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akitoa hotuba yake wakati wa hafla utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mabwawa  hayo.
Hafla ikiendelea.
Viongozi mbalimbali wakishuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mabwawa matatu  ya kutibu majitaka baina ya SUWASA
Wafanyakazi wa SUWASA wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (kulia) akisalimiana na Kaimu Afisa Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa SUWASA, Neema  Lulandala mara baada kuwasili katika hafla hiyo.
Picha ya pamoja
......................................
 Na Philemon Solomon, SINGIDA

MAMLAKA ya  Majisafi na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Singida (SUWASA) itajenga mabwawa matatu  ya kutibu majitaka baada ya serikali kuipatia mamlaka hiyo kiasi cha zaidi ya Sh.bilioni 1.7.

Mkurugenzi Mtendaji wa SUWASA, Sebastian Warioba, alisema hayo leo (13/10/2022) wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mabwawa hayo baina ya SUWASA na mkandarasi M/S Perntels Company and Nangai Engineering and Contractors Co.(T) Ltd na kushudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba.

Alisema kutokana na ongezeko la watu wanaofikia 193,116 katika Manispaa ya Singida imesababisha ongezeko la uhitaji wa maji linalofikia kiasi cha lita 15,063,048 kwa siku na hivyo kuwepo na ongezeko la uzalishaji wa majitaka ambao umefikia lita 12,803,519 kwa siku.

Alisema SUWASA imeamua kujenga mabwawa hayo hasa kutokana na kwamba  yasipodhibitiwa kwa wakati yanaweza kusababisha athari za kiafya na kimazingira kwa wananchi.

Warioba alisema mradi huo utakapokamilika utanufaisha wananchi 259,539 na pia utaboresha usafi wa mazingira na afya kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema SUWASA iweke mpango mkakati wa kuwa na mifumo ya ukusanyaji majitaka katika Manispaa ili kuwa na mji wa kisasa ambao unakidhi mahitaji.

Serukamba aliagiza SUWASA kuongeza wigo wa mtandao wa huduma za maji hasa maeneo ya pembezoni mwa mji na pia wadau wawe wanalipa Ankara za maji kila mwezi ili kuiwezesha SUWASA kumudu gharama za uendeshaji.

Post a Comment

0 Comments