Habari za Hivi Punde

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

BONANZA LA WAFANYAKAZI TANESCO MKOA WA SINGIDA 2024 LAFANA

Mkurugenzi wa Shirika  la Umeme Tanzania (TANESCO), Kanda ya Kati Mhandisi Danstan Ndamugoba akiwasalimia wachezaji wa Timu ya Muungano wa Wilaya wakati akifungua Bonanza la Wafanyakazi wa shirika hilo Mkoa wa Singida 2024 lililofanyika Uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida Oktoba 5, 2024.
Meneja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Mhandisi Mwamvita Ally akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo.

-----------------------------------------------

Imeandaliwa na  mtandao wa singidaniblog

BONANZA la Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Singida 2024 kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja limefanyika Uwanja wa Bombadia mjini hapa huku likihamasisha huduma bora na wateja wakitakiwa kuendelea kutumia nishati ya umeme na kuwa tayari kuilipia ili nao waendelee kuhudumiwa.

Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Shirika hilo Kanda ya Kati ambaye alikuwa mgeni rasmi Mhandisi Danstan Ndamugoba wakati akifungua Bonanza hilo ambalo lilihusisha michezo ya aina mbalimbali na kuwashirikisha wafanyakazi wa shirika hilo kutoka wilaya zote za Tanesco.

Ndamugoba alisema lengo la bonanza hilo ni kuongeza ushirikiano na umoja kwa wafanyakazi, kujuliana hali na kujenga afya zao na kuwa ili waweze kutoa huduma kwa wateja wao wanatakiwa kuwa na afya njema ambayo inapatikana kwa kufanya michezo.

“Tumekutana leo hapa kwenye bonanza hili na lengo lingine tukielekea kwenye wiki la huduma kwa wateja ambayo itaanza Oktoba 7, 2024 hadi Oktoba 14, 2024 sisi kama wafanyakazi wa Tanesco Mkoa wa Singida tukiwa sehemu ya wafanyakazi wa Kanda ya Kati tumeona tujumuike ili tutengeneze na kuimarisha afya zetu huku tukipendana na wiki ijayo tukaoneshe huduma bora tunazozizotoa kwa wateja wetu,” alisema Ndamugoba.

Alisema michezo hiyo haifanyiki kwa ajili ya wiki ya huduma kwa wateja tu bali ni endelevu na kuwa itakuwa ikiendelea kufanyika kwa dhima ya kuimarisha afya za wafanyakazi katika mikoa inayounda Tanesco Kanda ya Kati ambayo ni Morogoro, Dodoma na Singida.

Kwa upande wake Meneja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Mhandisi Mwamvita Ally alisema katika bonanza hilo wamekutana wafanyakazi  wa shirika hilo kutoka wilaya zote sita za Tanesco Mkoa wa Singida kwa ajili ya kujumuika pamoja kujuliana hali sanjari na kuimarisha afya zao kupitia michezo.

Mfanyakazi wa shirika hilo kutoka Manispaa ya Singida Ibrahim Solo alisema bonanza hilo ambalo limekuwa likifanyika kila mwaka limekuwa likiwaongezea ari na mori wa kufanya kazi na kubadilishana mawazo na wafanyakazi wenzao kutoka wilaya zingine ambapo alitumia nafasi hiyo kupongeza utaratibu huo.

Naye Grace Ngoi kutoka Manyoni alisema michezo hiyo wanayoifanya kupitia bonanza hilo imekuwa ikiwajenga kiakili na kimwili na kuwaongezea nguvu ya kufanya kazi pamoja na kuimarisha afya zao.

Katika bonaza hilo michezo ya aina mbalimbali ilifanyika kama ya kutembea na yai huku likiwa limewekwa kwenye kijiko ambapo mshindi aliyeibuka kidedea kwa upande wa wanaume alikuwa ni Bakari Athuman kutoka Wilaya ya Ikungi na kwa wanawake akiwa ni Sara Shalua kutoka Singida Mjini.

Katika shindano la kukimbiza kuku kwa upande wa wanaume mshindi alikuwa ni Issa Iddi kutoka Itigi na kwa upande wa wanawake akiwa Grace Ngoi kutoka Manyoni ambao waliondoka na kitoweo hicho.

Shindano lingine lililofanyika lilikuwa ni la kula tunda aina ya Aple ambapo kwa upande wa wanawake mshindi alikuwa ni Magreth Mtae kutoka Itigi na kwa wanaume alikuwa Salim Mbeto kutoka Manispaa ya Singida.

Mchezo wa kukimbia kwenye gunia mshindi kwa upande wa wanaume alikuwa Recardo  Fifi kutoka Ikungi na kwa upande wa wanawake akiwa Anna Juma kutoka Manispaa ya Singida huku mshindi wa kula mkate kwa kinywaji aina ya Pepsi akiwa ni Hamisi Mrisho kutoka Manispaa ya Singida.

Katika mchezo wa kuvuta kamba mshindi ilikuwa ni timu ya Kombaini dhidhi ya timu ya Tanesco Ofisi ya Mkoa wa Singida huku shindano la kuvaa soksi bila ya kuinama mshindi akiwa ni Mhandisi Boniface Shitindi.

Michezo mingine iliyofanywa katika bonanza hilo ni mpira wa miguu baina ya timu ya Muungano wa Timu za Wilaya dhidi ya Singida Manispaa ambapo timu ya Muungano wa wilaya iliibuka kwa ushindi wa mabao 2-1,  wakati mchezo wa Netball ushindi ukienda kwa timu ya Twiga kwa mabao 5-4 dhidi ya Timu ya Tausi.

Viongozi wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Timu za Muungano wa wilaya na Singida mjini..Timu ya Muungano wa wilaya ikiwa katika picha ya pamoja.na viongozi.Picha na wafanyakazi wa shirika hilo p.Meneja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Mwamvita Ally akirusha mpira gorini kuashiria kuzindua rasmi mchezo wa Netball kati ya Timu ya Taus na Twiga wakati wa bonanza hilo.
Mkurugenzi wa Shirika  la Umeme Tanzania (TANESCO), Kanda ya Kati Mhandisi Danstan Ndamugoba na Meneja wa Tanesco Mkoa wa Singida, Mwamvita Ally wakifuatilia kwa karibu michezo iliyokuwa ikiendelea uwanjani hapo.
Wafanyakazi wa shirika hilo wakiwa kwenye bonanza hilo.
Wafanyakazi wa shirika hilo wakiwa kwenye bonanza hilo.
Bonanza likiendelea.
Mfanyakazi wa shirika hilo, Siatu Mnanura akionesha umahiri wa kula tunda aina ya Aple wakati wa shindano la ulaji wa tunda hilo ambapo alikuwa mshindi wa pili..
Shindano la kula tunda la Aple kwa upande wa wanaume likifanyika.
Watoto wakiwa wamemzuia kuku kabla ya kuanza kwa shindano la kumkimbiza 
Shindano la kumkimbiza kuku likifanyika.
Mshindi wa kumkimbiza kuku kwa upande wa wanawake Grace Ngoi kutoka Manyoni akionesha furaha yake huku akiwa na kitoweo chake hicho.
Shindano la kuvuta kamba likifanyika.
Shindano hilo la kuvuta kamba likiendelea.
Shindano la kuvuta kamba kwa upande wa wanawake likifanyika.
Picha ya pamoja na viongozi ikipigwa.
Timu ya Singida mjini ikiwa katika picha ya pamoja..
Timu ya Muungano wa wilaya ikiwa katika picha ya pamoja.
Waamuzi wa bonanza hilo wakiwa tayari kwa kazi.
Mkurugenzi wa Shirika  la Umeme Tanzania (TANESCO), Kanda ya Kati Mhandisi Danstan Ndamugoba akiwasalimia wachezaji wa Timu ya Singida mjini.
Mashabiki wakifuatilia mpira wa miguu.
Mchezaji wa Timu ya Muungano wa wilaya, Recardo Fifi akimtoka mchezaji wa Timu ya Singida mjini   Elisante Chamshamu wakati wa bonanza hilo.
Mchezaji wa  Timu ya Singida mjini , Ibrahim Solo (kushoto) akimtoka  Edward Izango wa timu ya Muungano wa wilaya.

Post a Comment

0 Comments