Habari za Hivi Punde

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

DKT. MWIFUNYI: WATEJA WA MSD TUAMBIENI CHANGAMOTO ZENU TUBORESHE HUDUMA

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mtae kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Shafii Makamba (kulia) akitoa maelezo kwa Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi jinsi vifaa mbalimbali vilivyopelekwa kituoni hapo na MSD kupitia Serikali jinsi vinavyofanya kazi.

.............................

Na Dottoo Mwaibale, Lushoto

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi amewaomba wateja wa MSD kueleza  changamoto zao mbalimbali wanazokumbana nazo wakati wanapohudumiwa na MSD ili ziweze kuboresha huduma.

Dkt. Mwifunyi ameyasema hayo katika ziara yake ya kikazi mkoani Tanga alipokuwa akizungumza kwa nyakati tofauti na baadhi ya viongozi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Watumishi wa Kituo cha Afya cha Mtae ambacho kimepanda hadhi kutoa Zahanati baada ya kufanyiwa maboresho na kuanza kutoa huduma ya upasuaji.

“Tunawaomba muwe munatuambia changamoto mulizonazo wakati tukiwahudumia ili tuweze kuzifanyia kazi na wananchi waendelee kupata huduma bora kwani Serikali imekwisha jenga miundombinu pamoja na kuwezesha kupata bidhaa za afya,” alisema Mwifunyi,

Alisema katika ziara hiyo ameweza kuona matumizi ya mabilioni ya fedha yaliyotolewa na Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan jinsi yalivyofanya kazi kubwa kwa kujenga Kituo cha Afya cha kisasa Kata ya Mtae na kupeleka bidhaa za afya kupitia MSD zenye ubora wa hali ya juu.

Aidha, Dkt. Mwifunyi aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kwa kuwa kinara katika kulipa madeni ya fedha yanayotokana na bidhaa za afya wanazohudumiwa na MSD.

“MSD haiwezi kujiendesha bila ya kuwa na fedha mnapolipia madeni yenu kwa wakati yanaisaidia MSD iweze kufanya kazi vizuri ya kupata bidhaa za afya ambazo zinapelekwa sehemu mbalimbali hapa nchini kutoa huduma kwa wananchi,” alisema.

Kaimu Mganga wa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto Mohamed Almas, alipongeza MSD kwa kufanya mabadiliko makubwa ya usambazi wa bidhaa za afya na dawa ambapo alisema zamani bidhaa hizo zilikuwa zikiwafikia walengwa baada ya miezi miwili lakini hivi sasa ndani ya siku tatu au nne wanakuwa wamezipata.

“Zamani bidhaa hizo zilikuwa zikipitia Halmashauri za Wilaya na wao ndio walikuwa wakizipeleka kwenye vituo vya afya kupitia madaktari wa vituo vya afya, zahanati na hospitali hali ilikuwa sio nzuri hasa pale usafiri wa kuzipeleka ulipokosekana,” alisema.

Almas aliongeza kuwa utaratibu wa kutumia kompyuta na kuachana na matumizi ya karatasi umeleta maboresho makubwa ya upatikanaji wa bidhaa hizo za afya.

Kwa upande wake Mfamasia wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Rashida Ismail alisema maboresho ya usambazaji wa bidhaa za afya na dawa yanayoendelea kufanywa na MSD yamekuwa na tija kubwa kwani wakiaIuza vifaa hivyo wamekuwa wakivipata kwa wakati.

Alisema mbali ya kuvipata kwa wakati mawasiliano baina ya MSD na wateja wao ni mazuri ambapo ameeleza muda wote wanapowapigia simu kwa ajili ya kupata mahitaji hayo wamekuwa wakipatikana wakati wote.

 ziara hiyo ya Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Dkt.  Mwifunyi aliyoifanya na kufikia tamati Septemba 4, 2024 ilikuwa na lengo la kuzungumza na wateja wanaohudumiwa na MSD ili kupata maoni yao nini kifanyike ili kuendelea kuboresha huduma zinazotolewa na MSD na kupokea changamoto zao ili ziweze kufanyiwa kazi.

Aidha, ziara imekuwa ni sehemu ya ya kuadhimisha miaka 30 ya ufanyaji kazi wa MSD tangu ilipoundwa.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi, akiangalia vitanda vilivyopelekwa na MSD katika Kituo cha Afya cha Kata ya Mtae.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi akitoka kuangalia vifaa mbalimbali vya maabara vilivyotolewa na MSD kupitia Serikali.

Muonekano wa jengo la Utawala la Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto/


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa ziara hiyo. Kutoka kulia ni Mfamasia wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, RashidaIsmail, Mhasibu wa MSD Kanda ya Tanga, Grant Mwapele,  Meneja wa MSD Kanda ya Tanga, Sitti Abrahman, Afisa Huduma kwa Wateja MSD Kanda ya Tanga, Mary Isangu, Kaimu Afisa Huduma kwa Wateja MSD, Dkt. Pamella Sawa na Afisa Huduma kwa Wateja MSD, Gendi Machumani.
Kikao na Watumishi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mtae kikiendelea. Kutoka kulia ni Mganga Mkuu wa kituo hicho, Azizi Nanjasye, Muuguzi na Matroni wa kituo hicho, Josephine Nkya, Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Shafii Makamba, Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi na Meneja wa MSD Kanda ya Tanga, Sitti Abrahman.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ambaye pia ni Mlezi wa MSD  Kanda ya Tanga, Dkt. Rukia Mwifunyi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mtae na MSD baada ya ziara hiyo.
 

Post a Comment

0 Comments