Header Ads Widget

RC KATAVI AITAKA JAMII KUCHUKUA TAHADHARI YA MLIPUKO WA KIPINDUPINDU

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Januari 2, 2025.

...........................................

Na Mwandishi Wetu, Katavi 

MKUU wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ametoa mwezi mmoja kwa Katibu Tawala wa mkoa pamoja na wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Katavi kufanya ukaguzi wa kina kwenye maeneo ya biashara nakuchukua hatua za haraka Kuzuia magonjwa ya mlipuko ambayo tayari yameathiri maeneo mbalimbali ya mkoa wa Katavi.

Mrindoko ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kabla ya kuelekea katika gereza la mahabusu Mpanda kwaajili ya kukabidhi vitu mbalimbali ikiwemo mbuzi kwa lengo la kusherekea pamoja na mahabusu sikukuu za mwaka mpya.

Mbali na tahadhari ya magonjwa ya mlipuko pia Mrindoko amebainisha mambo mbalimbali ya kimaendeleo ambayo watayapa kipaumbele kwa mwaka huu 2025 ili kuboresha huduma kwa wananchi pamoja na kuinua uchumi wao na mkoa kwa ujumla.

Mrindoko amesema moja ya mambo ambayo watayaangalia kwa jicho la kipekee ni suala la umeme wa uhakika ili kuwapa fursa wananchi wandani na njee kuwekeza,

 

Post a Comment

0 Comments