WIZARA YA FEDHA YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI - MTAZAMO MEDIA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Sunday, 9 March 2025

demo-image

WIZARA YA FEDHA YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Responsive Ads Here

Wizara ya Fedha imeungana na Watanzania wengine kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, iliyofanyika kitaifa Jijini Arusha, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza maadhimisho hayo yakiwa yamebeba kauli mbiu ya ‘’Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji’’.

PICHA%201
PICHA%202
PICHA%203
Baadhi ya watumishi wanawake wa Wizara ya Fedha, wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, yaliyoadhimishwa kitaifa Jijini Arusha, yenye kaulimbiu ya ‘’Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji’’.
PICHA%204
Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza (kushoto), akitoa elimu ya fedha kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara, katika Maadhimisho ya Kimataifa ya Siku ya Wanawake Duniani, yaliyofanyika kitaifa katika Uwanja wa Sheikh Amiri Abeid, jijini Arusha. 
PICHA%205
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Usimamizi Rasilimali Watu Wizara ya Fedha, Bi. Fauzia Nombo (wa tatu kushoto) na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza (wa nne kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Fedha katika Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Siku ya Wanawake Duniani, yaliyofanyika Kitaifa katika Uwanja wa Sheikh Amiri Abeid, jijini Arusha.  
PICHA%206

Maafisa Hesabu Wakuu, Kitengo cha Huduma za Mfuko Mkuu (CFS), Wizara ya Fedha, Bi. Joyce Chacky na Bi. Mercelina Haule, wakitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maadhimisho ya Kimataifa ya Siku ya Wanawake Duniani, yaliyofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amiri Abeid, jijini Arusha

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Arusha)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages

Contact Form

Name

Email *

Message *