Gwaride maalumu likipita mbele ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akifunga Mafunzo ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi
la Polisi Tanzania Juni 9, 2025 Chuo cha Taaluma Kurasini Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa
amesimama wakati wimbo wa Taifa pamoja na ule wa Afrika Mashariki ukiimbwa mara
baada ya kuwasili katika viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Polisi kilichopo
Kurasini Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufunga Mafunzo ya Maafisa na
Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi Tanzania tarehe 09 Juni, 2025.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura wakati wa kufunga Mafunzo ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi Tanzania
katika sherehe zilizofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi kilichopo
Kurasini Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Juni, 2025.
















0 Comments