Viongozi
mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Kilosa wakimsikiliza Ndugu
Abdurahman Kinana wakati alipokutana nao leo katika mkutano wa ndani
mjini Kilosa
Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdurahman Kinana kulia akizungumza
na Mohamed Seif Khatib katikati na Mjumbe wa Katibu wa NEC Idara ya
Oganizesheni na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro
INNOCENT KALOGERIS mara baada ya kuwasili Wilayani Gairo wakitokea
Wilayani Kilosa ambako kabla ya kuondoka kulifanyika mkutano wa hadhara
katika uwanja wa Kilosa Town mjini Kilosa pia ilifanyika mikutano ya
ndani ambapo Katibu Mkuu aliongea na viongozi wa mashina, Madiwani
wenyeviti, wajumbe na waasisi wa chama hicho ikiwani pamoja na kufungua
mashina katika kuimarisha chama na kukagua baadhi ya shughuli za
maendeleo, kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi
Kikundi
cha ngoma za asili ya kabila la Wapogolo kikicheza ngoma hiyo kabla ya
kufanyika kwa mkutano wa hadhara katika uwanja wa Kilosa Town na
kuhudhuriwa na wananchi mbalimbali pamoja na wafuasi wa chama hicho
Kwaya ya CCM Kilosa ikiimba katika mkutano huo uliofanyika kwenye uwanja wa Kilosa Town leo. Nape
Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi chama cha Mapinduzi akiwahutubia
wananchi waliojitokeza katika uwanja wa Kilosa Town uliofanyika mjini
Kilosa leo Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdurahman Kinana akiwahutubia
wananchi waliojitokeza katika mkutano huo uliofanyika mjini Kilosa leo. Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdurahman Kinana akizungumza na
viongozi wa CCM Wilaya ya Kilosa katika mkutano wa ndani. Nape
Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi chama cha Mapinduzi akizungumza
na mmoja wa watoto waliohudhuria katika uzinduzi wa shina mjini Kilosa
Nape
Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi chama cha Mapinduzi akiwa amekaa
na akina mama kwenye mkeka huku akisaini kitabu cha wageni wakati wa
uzinduzi wa mashina mjini Kilosa
MASHINDANO YA NGUMI TEMEKE YAFANA INGAWA HAYANA WADHAMINI
Bondia Athumani Yanga wa timu ya Ashanti Boxing ya Ilala
Na mwandishi wetu
MASHINDANO ya klabu bingwa ya Mkoa wa Temeke yameanza jana jijini, Dar es Salaam huku yakishirikisha timu 20 na yanatarajiwa kufikia tamati Aprili 19 mwaka huu.
Lengo
la mashindano hayo yaliyoanza jana ni kuinua vipaji vya mabondia
chipukizi na kupata vipaji bora watakaokuwa chachu ya maendeleo ya
mchezo nchini.
Kocha
wa kimataifa wa mchezo huo nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ alisema
vijana wanakaoshiriki mashindano hayo walipima uzito katika Ukumbi wa
CCM Kata ya 15, Temeke Dar es Salaam.
Super
D ambaye pia ni kocha wa timu ya Mkoa wa Ilala ambao ni waalikwa katika
michuanohiyo alisema vijana wake kutoka klabu ya Amana na Ashanti
watafanya vema katika mashindano hayo.
Mkoa
wangu umetoa vijana sita ambao naamini watafanya vizuri katika
mashindano hayo kutoa upinzania mkubwa ambao utakuwa chachu ya maendeleo
ya mchezo huo nchini.
Super
D aliwataja baadhi ya mabondia hawo kuwa ni Hussein Mawimbi na Said
Hamisi kutoka klabu ya Amana na Athumani Yanga pamoja na Said Mabunda
kutoka klabu ya Ashanti.
Pia
aliwaomba wadau kujitokeza kusaidia mashindano hayo yanayofanyika
katika ukumbi wa CCM Kata ya 15, Temeke ili kuhakikisha hamasa ya
kuendeleza mchezo huo inapatikana yatakayofanikisha mafanikio ambalo
ndilo lengo kubwa. la mashindano hayo
Kocha
huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini, alisema kuwa katika mchezo
huo kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo huo zenye mapambano
makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza
kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo ni katika CD na DVD hizo ni ya Kalama
Nyilawila dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na Francis Miyeyusho,
Said Mundi na King Class Mawe. na Francis Cheka dhidi ya Japhet Kaseba
mapambano yote mawili mbali na hivyo atakuwa akisambaza vifaa vya mchezo
wa masumbwi kwa mabondia ambao awana wanaweza kumuona na kujipatia
vifaa mbalimbali
DKT BILALI AWATAKA VIONGOZI WA MAMLAKA ZA UDHIBITI NCHINI KUWA WAWAZI JUU YA KAZI ZA
Makamu wa Raisi Dkt Gharib Bilali amewataka viongozi pamoja na Mamlaka
za udhibiti hapa nchini kuhakikisha kuwa kabla hawajatoa maamuzi yao
wanawashirikisha wadau wao ikiwa ni pamoja na kuwa na tabia ya kuwa
wawazi ili kuweza kuboresha Mamlaka hizo.
Dkt Bilali aliyasema hayo mapema leo wakati akifungua mkutano wa
muungano wa mamlaka za Miundo mbinu barani Afrika (AFUM)
unaonendelea Jijini hapa.
Alisema kuwa kwa sasa kila mamlaka za usafirishaji zina takiwa
kuhakikisha zinajiwekea utaratibu wa kutotoa maaamuzi wanayotaka wao
wenyewe na badala yake wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanahusisha wadau
wote
Aliongeza kuwa endapo kama watakuwa na maamuzi yenye uwazi basi
yataweza kuharakisha maendeleo pamoja na wawekezaji hasa kwa nchi ya
Tanzania pamoja na barani afrika kwa ujumla hali ambayo nayo itaongeza
ufanisi kwenye mamlaka hizo za udhibiti.
“nawasisitiza kuwa uwazi na uwajibikaji ndio sehemu pekee ya kuwafanya
muwe na sifa nzuri lakini hata kukwepa lawama kwa wananchi lakini pia
ninyi kama ninyi mna nafasi kubwa sana ya kuhakikisha kuwa mnaongeza
ubora wa mamlaka zenu jamani “aliongeza Dkt Bilali
Awali dkt Bilali alimpongeza waziri wa Nchi ofisi ya raisi Dkt Mark
Mwandosya kwa kutoa kitabu ambacho kinaoenesha na kufafanua juu ya
masuala mbalimbali yanayohusu masuala yanayohusu mamlaka za udhibiti
hapa nchini
muungano wa mamlaka za Miundo mbinu barani Afrika (AFUM)
unaonendelea Jijini hapa.
Alisema kuwa kwa sasa kila mamlaka za usafirishaji zina takiwa
kuhakikisha zinajiwekea utaratibu wa kutotoa maaamuzi wanayotaka wao
wenyewe na badala yake wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanahusisha wadau
wote
Aliongeza kuwa endapo kama watakuwa na maamuzi yenye uwazi basi
yataweza kuharakisha maendeleo pamoja na wawekezaji hasa kwa nchi ya
Tanzania pamoja na barani afrika kwa ujumla hali ambayo nayo itaongeza
ufanisi kwenye mamlaka hizo za udhibiti.
“nawasisitiza kuwa uwazi na uwajibikaji ndio sehemu pekee ya kuwafanya
muwe na sifa nzuri lakini hata kukwepa lawama kwa wananchi lakini pia
ninyi kama ninyi mna nafasi kubwa sana ya kuhakikisha kuwa mnaongeza
ubora wa mamlaka zenu jamani “aliongeza Dkt Bilali
Awali dkt Bilali alimpongeza waziri wa Nchi ofisi ya raisi Dkt Mark
Mwandosya kwa kutoa kitabu ambacho kinaoenesha na kufafanua juu ya
masuala mbalimbali yanayohusu masuala yanayohusu mamlaka za udhibiti
hapa nchini
Alisema kuwa Kitabu hicho ambacho kimeandaliwa na Waziri huyo
kinatakiwa kutoa elimu kwa wananchi pamoja na mamlaka hizo za udhibiti
kwa kuonesha changamoto pamoja na suluhu ambazo wakati mwingine
zinachangia sana maendeleo ya nchi
kinatakiwa kutoa elimu kwa wananchi pamoja na mamlaka hizo za udhibiti
kwa kuonesha changamoto pamoja na suluhu ambazo wakati mwingine
zinachangia sana maendeleo ya nchi
Awali Profesa Mwandosya alisema kuwa kitabu alichokiandaa ambacho
kinahusu masuala ya udhibiti wa Mamlaka pia kinaweza kutumika na watu
wote hasa wananchi ambao wakati mwingine wanashindwa kujua na
kuzielewa kazi maalumu za mamlaka hizo ndani ya nchi husika
kinahusu masuala ya udhibiti wa Mamlaka pia kinaweza kutumika na watu
wote hasa wananchi ambao wakati mwingine wanashindwa kujua na
kuzielewa kazi maalumu za mamlaka hizo ndani ya nchi husika
Mbali na hayo alisema kuwa Kitabu hicho pia kitaweza kuwafikia
wanafunzi hasa wale wa masomo ya biashara ambao wataweza kujifunza na
kisha kuona jinsi ambavyo wataweza kusaidia jamii zao
wanafunzi hasa wale wa masomo ya biashara ambao wataweza kujifunza na
kisha kuona jinsi ambavyo wataweza kusaidia jamii zao
WABUNGE WASHAURIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA KUHAMASISHA WANANCHI KUJIUNGA NA KUANZISHA BENKI ZA JAMII
Na Benedict Liwenga-Maelezo, Dodoma.
SERIKALI
inahakikisha kuwa inaweka mazingira bora na salama ya kiuchumi ili
kuwezesha sekta binafsi kuanzisha mabenki na kutoa huduma bora za
kibenki kwa wananchi.
Hayo
yamesemwa leo Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na
majibu ambapo Mbunge wa Kwela Mhe. Ignas Aloyce Malocha aliuliza swali
kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha akitaka kujua ni lini Serikali
itashawishi taasisi za kifedha kuanzisha matawi yao katika mji mdogo wa
Laela.
Naibu
Waziri Fedha Mhe. Saada Mkuya Salumu kwa niaba ya Waziri Fedha alisema
kuwa serikali inatambua umuhimu wa wananchi kupata huduma za kibenki
karibu na maeneo yao na pia serikali inatambua kuwa huduma hizo za
kibenki kwa wananchi kazima ziwe zenye faida kwa pande zote mbili yaani
kwa mabenki na wateja.
Naibu
Waziri aliongeza kuwa kwa kuzingatia sera ya sasa ya huduma za mabenki,
waheshimiwa Wabunge wanaweza kushirikiana na Serikali katika
kuwahamasisha wananchi kujiunga na kuanzisha benki za jamii (Community
banks) zinazozingatia mazingira ya mahali husika pamoja na kuzihamasisha
benki zilizopo nchini kufungua matawi katika maeneo hayo.
“Serikali
kwa kutambua umuhimu wa suala hili, imewasiliana na Benki ya NMB ambao
wamekubali kwenda Laela kutathmini mazingira ya kibiashara kabla ya
kufungua tawi mahali hapo”. Alisema Naibu Waziri huyo.
Akijibu
maswali mawili ya nyongeza toka kwa mbunge huyo ambayo yalitaka kujua
kwanini serikali isitumie Mobile Banking na kwanini benki hutoza riba
kubwa, Mhe. Mkuya alijibu kwa kusema kuwa serikali haitumii mobile
banking hivyo itashawishi benki nyingine zianzishe huduma hizo.
Kuhusiana
na riba kubwa itozwayo na mabenki, Naibu Waziri alisema kuwa riba kubwa
inategemea na benki zenyewe zinavyotumia gharama kubwa na riba katika
kutoa huduma hivyo nao hawanabudi kupandisha riba kwa wateja wao.
Serikali
kupitia Benki Kuu, imeweka sheria na taratibu za kusaidia juhudi za
wananchi katika kuanzisha mabenki au taasisi za fedha katika maeneo yao.
Serikali pia inayo sera ya Taifa inayolenga kuhamasisha uanzishwaji wa
mabenki kwa ajili ya wateja wadogo (National Microfinance Policy) na
sera hii inasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania.

0 Comments