Random Posts

LUIS SUAREZ KIFUNGO MECHI 10!!, BALAA LINGINE KWA MAJOGOO WA JIJI!!

LUIS SUAREZ KIFUNGO MECHI 10!!, BALAA LINGINE KWA MAJOGOO WA JIJI!!

Baraka Mpenja wa Fullshangwe kwa msaada wa Sportsmail.com
Mshambuliaji nyota wa Liverpool, Luis Suarez, leo amepewa Adhabu ya Kufungiwa kutocheza Mechi 10 na FA, Chama cha Soka England, kwa Kosa la kumng’ata meno Beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic, kwenye Mechi kati ya Liverpool na Chelsea iliyochezwa Jumapili iliyopita.
Katika Mechi hiyo ambayo ilitoka 2-2, Refa Kevin Friend hakuliona tukio hilo lakini Ivanovic alilalamika kwa Refa na kumuonyesha mkono wake ulioumwa.
Mara baada ya Mechi hiyo Suarez aliomba radhi na Klabu ya Liverpool ilimpiga Faini.
Baada ya FA kupata Ripoti ya Refa Friend, ambae alikiri kutoliona tukio hilo, njia ikawa wazi kwa FA kumfungulia Mashitaka Suarez ambae alikiri Kosa lakini aliomba Adhabu yake ibakie Kifungo cha Mechi 3.
Ikitoa Adhabu hiyo, Jopo Huru la FA lilikubali Kifungo cha kawaida cha Mechi 3 kwa Kosa la kuleta vurugu na kuongeza Mechi nyingine 7 kwa kuzingatia uzito wa kosa lenyewe la kinyama.
Adhabu hiyo inaanza mara moja ikimaanisha Suarez atazikosa Mechi zote 4 Liverpool ilizobakisha kwa Msimu huu pamoja na Mechi zao 6 za kwanza za Msimu mpya wa 2013/14 utakaoanza Mwezi Agosti.
Suarez amepewa hadi Ijumaa hii Saa 9 Mchana, Bongo Taimu, kukata Rufaa ikiwa hakuridhika na Adhabu.
I'm back: Luis Suarez returned to training today while the FA deliberated over his punishment for biting
Nimerudi: Luis Suarez akiwa mazoezini leo hii baada ya FC kumfungia mechi 10
Bite club: Suarez sunk his teeth into Branislav Ivanovic during the Premier League match at Anfield
 Suarez akizamisha meno yake katika mkono wa beki wa Chelsea Branislav Ivanovic wakati wa mechi yao ya ligi kuu uwanjani Anfield.

tasty: The bizarre clash was missed by referee Kevin Friend, who had to be told the specifics by Ivanovic
Mwamuzi wa mchezo huo Kevin Friend akiambiwa na Ivanovic kwamba Suarez kaning`ata 

tasty: The bizarre clash was missed by referee Kevin Friend, who had to be told the specifics by Ivanovic

Ivanovic akiwa amkeaa chini kuugulia maumizi ya kung`ata na Surezi.
VIFUNGO VIREFU TOKA FA:
-MIEZI 9: Mchezaji wa Manchester United Eric Cantona kwa kumpiga Mshabiki Mwaka 1995
-MIEZI 9: Kipa wa Chelsea Mark Bosnich kwa kugundulika kutumia Kokeni Mwaka 2003
-MIEZI 8: Rio Ferdinand wa Manchester United kwa kukosa kupimwa utumiaji Madawa yanayokatazwa hapo Mwaka 2003
-MECHI 12: Joey Barton wa QPR kwa kuleta vurugu kwenye Mechi na Man City Mwaka 2012.
-MECHI 11: Paolo Di Canio alipokuwa Sheffield Wednesday kwa kumsukuma Refa Paul Alcock Mwaka 1998
-MECHI 10: David Prutton wa Southampton kwa kumsukuma Refa Alan Wiley Mwaka 2005
-MECHI 10: Luis Suarez kwa kumuuma Branislav Ivanovic Mwaka 2013
-MECHI 9: Paul Davis wa Arsenal kwa kumpiga ngumi Glenn Cockerill wa Southampton Mwaka 1988 na kumvunja taya.
-MECHI 8: Luis Suarez kwa kumkashifu Kibaguzi Patrice Evra Mwaka 2011
-MECHI 8: Ben Thatcher wa Man City kwa kumpiga kipepsi Pedro Mendes wa
Portsmouth Mwaka 2006.
-MECHI 5: Roy Keane wa Man United kwa kuandika maneno yasiyokubalika kwenye Kitabu chake hapo Mwaka 2002

JKT RUVU YAWAFUMUA LYON 1-0 CHAMAZI, MNYAMA VS RUVU SHOOTING KIMBEMBE KINGINE KESHO TAIFA!!


1

Baada ya kufumuliwa mabao 3-0 na vinara wa ligi kuu soka Tanzania bara Dar Young Africas, leo hii maafande wa JKT Ruvu wamepunguza machungu baada ya kuwatungua vibonde wa ligi hiyo Africa Lyon bao 1-0 mchezo uliopigwa dimba la Chamazi jijini Dar es salaam.
Kocha msaidizi wa JKT Ruvu Greyson Haule alisema wapinzani wao  leo wamecheza vizuri sana lakini bahati katika mchezo huo iliangukia upande wao.
“Hakika mchezo ulikuwa mgumu, lakini kiwango cha timu yangu kinaniridhisha siku hadi siku licha ya kuachwa na kocha wetu Charles Kilinda, lakini sasa tunaye mwalimu Keny Mwaisabula ambaye kiukweli kachangia mambo mengi sana” . Alisema Haule.
Haule aliongeza kuwa kushinda mchezo wa leo ni hatua kubwa kwao kwani wanajipa matumaini mazuri ya kufanya vizuri mechi zilizosalia.
Kocha huyo alisema sasa hesabu zao ni mchezo ujao dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons “Wajelajela” ambao wanajiandaa kunyakua mzigo wa pointi tatu muhimu.
“Tunajiandaa kufanya vizuri na lazima shughuli iwe nzito na Prisons, tuna morali kubwa na mashabiki wetu wasiwe na wasiwasi kwasababu tuna uhakika wa kubakia ligi kuu msimu huu”. Aliongeza Haule.
Baada ya shughuli ya leo Taifa, hapo kesho kibarua kingine ni kati ya wekundu wa Msimbazi Simba watakaowakaribisha maafande wa Ruvu Shooting kutoka mkoani Pwani katika dimba la taifa.
Kuelekea katika mchezo huo, kocha msaidizi wa klabu ya simba, Jamhuri Kiwhelo Julio alisema wachezaji wote wapo salama na wanajiandaa kukumbana na wanajeshi hao ambao wako sawa kwa kila idara”.
“Shooting ni timu nzuri na kila mtu anajua, matokeo yoyote yatakayopatikana tutamshukuru Mungu, wachezaji wanajua ugumu wa mechi lakini kocha Liwieg kushirikiana na mimi tumefanya maandalizi kwa wachezaji wetu”. Alisema Julio.
Julio alisema kufungwa ni jambo la kawaida katika mchezo wa soka huku akitolea kipigo cha jana walichokipata Barcelona kutoka kwa Bayern Munich cha mabao 4-0.
“Jana kila mtu alikuwa anashangaa, lakini soka ni mchezo wa mahesabu, ukikosea unapigwa, na ndio maana jana Barca walicheza ovyo wakapigwa kipigo cha mbwa mwizi, na sisi tukifungwa sio ajabu”. Alisema Julio.
Kocha huyo aliwataka mashabiki wa simba kuwaombea dua njema wachezaji wao ili waamke salama hapo kesho, lakini pia wajitokeze uwanjani kuwashangilia vijana wao.
Kwa upande wa Ruvu Shooting, afisa habari wa klabu hiyo Masau Bwire alisema wamejiandaa kuwafunga simba wanaosikika wakisema wanataka kulinda heshima mechi zilizosalia baada ya kupoteza ubingwa wao msimu huu..
“Tumesikia maneno ya wana Simba kuwa wanataka kutufunga na kulinda heshima, mwalimu Mkwasa mnamjua, kafanya mambo yake na kesho mnyama hatoki kwetu”. Alijigamba Masau.

JENGENI TABIA YA KUPIMA UGONJWA WA KISUKARI- DK. MWINYI

1
 Dk. Hussein Mwinyi
NA MAGRETH   KINABO – MAELEZO
IMEELEZWA kwamba  inakadriwa  kuwa asilimia saba ya idadi ya watu wazima wanaugua ugonjwa wa kisukari, lakini chini ya 1/3  ndio wanaofahamu  wana tatizo hilo.
 Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein   Mwinyi wakati akizindua kliniki  ya vikoba ya wagonjwa wa kisukari uliofanyika  kwenye viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dares Salaam.
 Dk. Mwinyi alisema watu wanaokabiliwa na tatizo hilo, wanafika hospitalini wakiwa  wameathirika figo, macho, shinikizo la damu au kukatwa miguu.
“ Ninaishauri jamii kutumia huduma hiyo ili kuweza kuchunguza  afya zao na kujinga  kwa kufuata kanuni za afya  kama vile kula vyakula visivyo na mafuta mengi, sukari nyingi, chumvi kiasi, kula mboga za majani kwa wingi na matunda,” alisisitiza. Dk. Mwinyi.
  Aliongeza pia jamii inatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha, kupunguza uzito kwa kiwango kinachotakiwa, kutovuta sigara na kupunguza kunywa pombe au kuacha kabisa.
 Dk.Mwinyi alisema 1/3 ya idadi ya watu wazima wanakabiliwa  na shinikizo la damu, lakini chini ya asilimia 10 ndio wanafahamu kuwa wameathirika na tatizo hilo. 
 Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Wagonjwa wa Kisukari   Tanzania, Dk.Kaushik Ramaiya alisema kliniki hiyo imezinduliwa kwa ushirikiano wa chama hicho na wizara hiyo ili kuboresha huduma za afya nchini.
 Pia imetolewa na  Novo   Nordisk wakishikikiana na Chama cha Wagonjwa wa Kisukari Duniani.
 Alisema  kliniki hiyo  ambayo itakuwa na  inatoa tiba kwa wagonjwa wa   kisukari   hususan watoto inafaa vifaa vya  kisasa kwa ajili ya upimaji wa matatizo ya  kisukari ,macho,meno na mahabara ikiwemo  genereta  itakatotumika  sehemu ambazo hazina umeme . Pia  itatoa huduma  hiyo kwa watu wazima .
  Aliongeza kuwa kliniki hiyo ni ya kwanza kuzinduliwa  ni  maalum kwa kanda ya ziwa ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi. Hivyo hapo baadae watatoa nyingine kwa ajili ya kanda  zingine.
 Katika uzinduzi huo jumla ya watu wapatao 79 walijitokeza kupima afya zao na kupata ushauri mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments