Baadhi ya watoto ombaomba wakiwa wamelala kama walivyo kutwa na mpiga picha wetu eneo la kisutu jijini Dar es salaam leo huku tatizo la watoto wa mitaani likizidi kushika kasi kila kukicha
PICHA NA BERNARD JAMES WA MTAZAMO MEDIA DAR ES SALAAM
Na Bernard James wa Mtazamo Media Dar es salaam
Na Bernard James wa Mtazamo Media Dar es salaam
Watoto wadogo wanao tumiwa na wazazi wao kuomba katika mitaa
mbalimbali jijini Dar es salaam limezidi
kuongezeka na kushika kasi kila kukicha huku vyombo husika vikiwa kimya kama
vile hakuna tatizo.MTAZAMO limegundua upashanaji habari zakuitana kuja jijini kwa
wazazi wanaowatumia watoto wao wadogo kuomba na wale ambao wako mikoani hasa
mkoa wa Dodoma kuja jijini Dar Es Salaam na kwamba hakuna usumbufu,akiongea kwa
masikito MR Munis ambae ni Dalali katika
soko la Ndizi Mabibo ameshangazwa na Wizara husika kutochua hatua kwa kuwakata
na kuwarudisha makwao wazazi wanao watumia watoto kuomba omba ,huku wakionekana
wanao uwezo wakufanya kazi,angalia hali ilivyo je?hawa watoto wanakosa haki yao
ya msingi ya kupata Elimu,alisema Munis
0 Comments