Random Posts

WACHINA TISHIO KWA TAIFA NA RASILIMARI ZAKE


Pamoja na kelele zote za kupinga ujangili nchini .Wachina wameziba masikio.wameendelea kuuwa Tembo bila huruma.kwa raia wa China  kwa mwanvuri wa uwekezaji imekuwa pigo kwa mariasili ya wanyama pori wetu.kitu kinacho hatalisha kutoweka kwa rasili mali za wanyama wetu wa porini,Tembo sasa yuko hatalini kutoweka iwapo hazitafanyika jitihada .Wachina wakishilikiana na Watanzania baadhi wamekamatwa kwa utoroshwaji wa Meno ya Tembo na Madini aina ya Tanzanite. Kwa kutumia meri ya kivita ya Kichina iliyotia nanga hivi karibuni.ktk bandari ya Dar Es Salaam.tukio la kukamatwa kwa pembe za Tembo lilitokea juma tatu ya23/12/2013 Saa3 usiku wakati gari moja binafsi ilipo fika gate No2 ikisindikizwa na gari la Polisi.huku ndani yake kukiwa na polisi.wakitaka kufika gate N O3Iliko manowari ya kichina katika gari la kiraia kulikuwa na Raia 3 wa kichina.wa2 wakiwa wana jeshi na mmoja raia wakawaida wa china,pamoja na dereva ambae ni raia.walinzi wa gate no2 walilazimisha kulikagua lile gari.kitu kilicho sababisha kutokea mabishano makari.ndipo zilipokutwa shehena kubwa ya meno ya tembo.Wachina walitoa milion25 za kiTanzania kwa lengo la kuw honga walinzi,kitu kilchokataliwa na walinzi.kuona hivyo Wachina walitimua mbio kuelekea kwenye meli yao.hata hivyo walikamatwa pamoja na shehena ya nyara za Taifa ambayo thamani yake bado tathimini haijafanyika.wakati wa kuuaga mwaka2013 na kuukaribisha 2014 .Mhe, Rais wa Jamuhuri ya Tanzania aliongelea Tatizo la ujangili nchini kwa hisia kari.na jinsi operation Tokomeza Ujangili ilivyofanikiwa.na baadhi ya silaha za kivita walizokuwa wanatumia majangili kukamatwa na baadhi ya watumishi wa wizara ya mariasili waliokuwa wanashilikiana na majangili kukamatwa.na kwamba katika pori la akiba la selous tembo wmepungua kwa kiasi kikubwa kutoka Tembo109.419 mwaka 1976-Tembo 13.084 mwka2013.hili ni tatizo kubwa sana.Wachina ni tatizo kubwa hapa Tanzania.wananchi wanaoishi kandokando ya mbuga za wanyama na mapori ya akiba wameingia katika mtego wa waWachina.wameahidiwa kwa kila jino moja la Tembo shilling laki moja/100.000 .kwa mwananchi wa kijijni sh 100.000 kwa kila jino ni pesa nyingi sana.wameamua kutumia maboga yenye sumu kuwa uwa Tembo kwa ajili ya meno yao.na kuna meno mengi yamefukiwa ardhini baada ya operation tokomeza ujangili kuanza.kuna haja kubwa kupitisha elimu kwa jamii umuhimu wa kuzilinda mariasili zetu.na mazingila yake

Post a Comment

0 Comments