Random Posts

KAMPUNI YA MABIBO BEER WINES AND SPRITS KUDHAMI MBIO ZA MWENGE WA UHURU ZITAKAZOFANYIKA MKOANI KAGERA



Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits, James Rugemarila (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe alipowasili katika ofisi za Kampuni ya Mabibo Aprili 10, 2014 jijini Dar es Salaam,kwaajili ya kuzungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maandalizi ya Uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru zitakazozinduliwa kitaifa katika Mkoa huo ambapo uzinduzi huo utaenda sambamba na uzinduzi wa miradi mbalimbali katika mkoa huo.wadhamini wa  mbio hizo ni Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits.

HABARI PICHA-NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWEBLOG DAR ES SALAAM
0787 94 2222


Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Sprits,Benedicta Rugemalira (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe, alipowasili kuzungumza na waandishi wa habari.

Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe (katikati), Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits, James Rugemarila, na kushoto, Mkuu wa Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, Lembris Kipuyo wakiingia kwenye ukumbi ulioandaliwa kwaajili ya kuzungumza na waandishi wa habari.

Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits, James Rugemarila,akielezea machache kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe, kuhusiana na kuadhamini kwa mbio za Mwenge wa Uhuru.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe (katikati), akizungumza na waandishi wa habari kuhusina na maandalizi ya Uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru zitakazozinduliwa kitaifa katika Mkoa huo ambapo uzinduzi huo utaenda sambamba na uzinduzi wa miradi mbalimbali katika mkoa huo.wadhamini wa  mbio hizo ni Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits.

Mkuu wa Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, Lembris Kipuyo akisisitiza kuhusina maandalizi yam bio hizo, kulia kwake ni, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe: Fabian Masawe,

Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Sprits,Benedicta Rugemalira, akielezea kuhusiana  na jinsi walivyo jiandaa kuhusina na mbio za Mwenge wa Uhuru.


Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits, James Rugemarila, akisisitiza jambo.


Meneja Mauzo wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits, Bw Kevin Costa akitambulisha wageni mbalimbali wakati wa mkutano huo.


Waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo.


Meneja Masoko na Biashara wa Benki ya Mkombzi, Grace Mboya akielezea kuhusina huduma za kibenki wakati, kushoto kwake ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Sprits,Benedicta Rugemalira

Kulia ni Bw: Boniface, na Rutabingwa, wakimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, Lembris Kipuyo wakati akiezea kuhusiana na maandalizi ya Uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru.

Joe Mgaya (kushoto), akiwa na Respicus Didace, wakifurahia jambo wakati wa Mkutano huo.

wafakazi wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spririt, wakiwa kwenye Mkutano huo.
 ........................................................................................


Dar es Salaam.Mkoa wa Kagera unategemea kutumia Bilioni 14 kwa ajili ya kuzindua miradi mbalimbali wakati wa kukimbiza mbio za Mwenge wa Uhuru utakaozinduliwa  Kitaifa Mei 2 mwaka huu.
Hayo yalibainishwa na Mkoa huo, Fabian Masawe wakati akizungumza na waandishi wa Habari jana kuhusu maandalizi ya uzinduzi  huo.
Alisema mwenge huo utakimbizwa katika halmashauri nane za mkoa huo ambapo  wananchi zaidi ya 30,000 watashiriki wakiwemo kutoka nchi za jirani na mkoa huo.
Masawe alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kujitokeza kuchangia mbio hizo ili kukufanikisha uzinduzi  huo.
Alisema baada ya kukimbiza katika Halmashauri hizo kuwa mwenge huo  Mei 10 mwaka huu utakabidhiwa katika wilayani Kakongo mkoani Kigoma.
“Kauli mbiu ya mwaka huu yam bio za mwenge Katiba ni Sheria kuu ya nchi jitokeze kupiga kura ya maoni kupata katiba mpya”,alisema Masawe.
Mdhamini wa mbio hizo,Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spririt,Benedicta Rugemalira alisema watashirikin na Serikali kudhamini sehemu y uzinduzi  huo kupitia vinywaji vyao.
Rugemalira alisema watahakikisha wanatoa huduma za vinywaji kambacho hakina kilevi na bia ya Windhoek.
“Vinywaji hivi ni vizuri sana hivyo wananchi watafurahia sana wakati wa uzinduzi wa mbio za mwenge utakaofanyika mkoani Kagera"