Random Posts

MAJANGILI HAWATAPATA NAFASI YA KUKANYAGA NA KUPUMZIKA



Na Bernard James
+255 752106535
…………………………….
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe:Lazaro Nyalandu akizungumza na waandishi wa habari  hivi karibuni jijini Dar es Salaam,  alisema majangili hawana nafasi tena ,na hawana pa kukanyaga katika nchi za Afrika mashariki na watanaswa wote,aliyaongea hayo wakati wa mkutano wa wadau wa kimataifa na Serikali waliokutana  kuweka mikakati yanamna ya kuzuia ujangili wa wanyamapori na hasa Tembo, ambao wapo hatarini kutoweka kutokana na majangili   kuwawindana kuwaua kwa ajili ya kuchukua meno yao, ambayo yana soko kubwa katika nchi za Mashariki ya mbali hasa China na Vietinamu,
Tanzania imefanya kila juhudi ya kuutokomeza ujangili ,rakini jitihada hizo haziwezi kufanikiwa bila waTanzania wote wenye mapenzi mema kushilikiana pamoja, Wizara ya maliasili pekee haiwezi kumaliza tatizo hili bila kuunganisha nguvu zetu pamaoja, nakuanzia sasa baadhi ya Wizara zitashilikiana na Wizara ya maliasili katika kuunda kikosi kazi,ikiwemo Wizara ya Mambo ya ndani,Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Maliasili na utalii yenyewe.
Pia Nyalandu alisema Wizara imeanzisha mamlaka ya Wanyamapori na,  itajenganyumba za wafanyakazi na Morogoro ndio itakuwa makao makuu ya mamlaka ya wanyamapori (TAWA)   ambayo wafanyakazi 70% kuhamia baada ya majengo kukamilika.
Mkutano huo wa wadau wa Kimataifa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili ulifanyika siku mbili 2 katika Hotel ya Kimataifa yaHyatt Regency,ambao uliandaliwa na The ICCF Group
Waziri Nyalandu ambae ni mwiba mkari kwa majangili  nchini ,Majangili wamejiunga kwa pamoja nakuweka mikakati ya kumkwamisha Nyalandu katika jitihada zake za kuutokomeza ujangili,mikakati hiyo inalatibiwa na aliyewahi kuwa Waziri katika Wizara hiyo ya maliasili akishilikiana na baadhi ya wafanyabiashara ya utalii na wamiliki wa baadhi ya vitalu vya uwindaji,walengwa wakubwa katika mikakati hiyo ni Mhe,Lembeli,Nyalandu,na Sarakikya ambae ni kaimu mkurugenzi wa Wanyamapori,mikakati hiyo nipimoja nakutolewa kwenye magazeti kurasa za mbele kila wiki ,kwakuwabambikizia tuhuma mbalimbali,ikiwemo Nyalandu kumihusisha na ujangili na CIA na Uraia wa Marekani,mikakati hiyo lengo lake kumfanya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano kumuondoa katika nafasi hiyo.   Baadhi ya wamiliki wa vitalu nchini na baadhi ya wenye makampuni ya Utalii nchini wamekuwa wakihusishwa katika ujangili wa Tembo na wanyama wengine,hutumia mwanya wa kukata vibari vya wanyama kwa idadi furani,rakini wakifika porini wanauwa wanyama zaidi ya idadi waliyolipia,Baadhi ya majangili wamebuni mbinu mpya wameweza kujipenyeza mpaka kwenye jumuiya za wanavijiji wanaopakana na mbuga za wanyama ,mpori ya akiba,na tengefu na kuwawafazirili  wa jumuiya hizo ilikuficha madhambi yao,pia wameweza kujipenyeza mpaka kwenye chama cha mapinduzi ccm nakuwa viongozi,na  wafadhili,hii yote katika kuficha makucha ,yao kitu ambacho ni hatali kwa ustawi wa malisili zetu ,tukidanganyika nao na ufadhili uchwara wao.
pia Nyalandu alitangaza kufanyika kwa mkutano mkubwa nchini Nov 7-8-2014 utakao kutanisha maTaifa  majilani zetu Nchi za Malawi, Zambia, Uganda Msumbiji ,Mkutano huo utajadili mauaji ya Tembo kwa nchi hizo na namna ya  kudhibiti majangili ambao uhamahama pindi wanapofanya uhalifu na kukimbilia nchi moja wapo,maana majangili wanafahamiana nikama wafanya biashara ya madawa ya kulevya,pia viongozi wa Dini watashirikishwa aliongeza Nyalandu,na tarehe4/11/2014 utafanyika mkutno mwingine wa ki-Mataifa kujadili ujangili,ambao bado haujaisha.
Katika mkutano huu uliomalizika alhamis 9/9-2014 Wadau mbalimbali wa kimataifa walishiriki wakiwemo ma-barozi mbalimbali na mashirika ya kifedha na Taasisi  Barozi wa China  Mr Lu Youging aliahidi nchi yake kutoa msaada wa vitendea kazi yakiwemo magari,pia china itatoa mafunzo na ushauli mbalimbali kwa Tanzania Barozi Lu alisema China inauzoefu wa miaka40 wakukabiliana na ujangili nchini mwao ,ambapo wanyama aina ya Panda na Tiga walikuwa wapo hatalini kutoweka China, rakini China iliweza kuidhibiti hali ya ujangili na kila jangili aliyekamatwa alipewa adhabu kali ,kitu kilichopelekea kukomesha ujangili,pia Lu aliahidi kuyayashauli makampuni ya china yaliyopo nchini kusaidia kutoa misaada mbalimbali itakayohitajika,makampuni hayo ni yale ya ujenzi na Huawei,pia atayashauli makampuni ya  China yaje kuwekeza katika utalii nchini ilikuongeza pato lamtu masikini na kuwa mtu mwenye kipato cha wastani  kitu kitakachowafanya wasiji-ingize katika ushawishi wakufanya ujangili ,
Nae  mbunge wa Iringa ambae pia ni Waziri Kivuli wa Maliasili kambi ya upinzani ,Aliipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii katika jitihada zake kubwa za kuhakikisha ujangili unatoweka nchini,mapambano dhidi ya ujangili sio ya Nyalandu,ccm,cuf wala chadema bali ni ya kila M Tanzania,hii ni vita kama ile ya kumuondoa nduli Idi Amini wa Uganda ambapo waTanzania wote tuliungana katika kumpiga Nduli,kambi ya upinzani inapongeza jitihada zote zinazofanywa na Nyalandu kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali.aliviomba vyombo vya habari nchini kuunga mkono jitihada hizo zinazofanywa na Serikali kwa kuandika mambo ya ukweli na kutia nguvu kwa wale wote wanaofanya juhudi katika kutokomeza ujangili ambayo Waziri ameonyesha kuzifanya na ziko wazi.
Msigwa aliongeza kwa kusema sasa uzalendo uwe mbele kwa kila mTanzania ,haiwezekani yakaja majangili yakafanya ujangili bila kushilikiana na WaTanzania wenyewe na ndio wanaowaonyesha njia zote zakupitia katika kutekeleza ujangili huo alionya Msigwa.