![]() | |||||
| Na Bernard James-+255752106535 |
Shule za St Mary
zinazomilikiwa na Dr Mama Rwakatale na Filbert Bay zimeshuka kitaaluma hivyo
kusababisha wazazi wanaosomesha watoto katika shule hizo kuwahamisha watoto wao
katika shule nyingine imefahamika.
Tofauti na katika
miaka ya 2000 ambapo kila mzazi aligombea nafasi katika shule hizo ili mtoto wake
asome hapo,
Katika mahafali ya 13
ya kuwaaga wanafunzi wanaomaliza katika shule ya Filbert Bay,Mkurugenzi wa
shule hizo na mmiliki Anna Bayi alitumia muda mwingi kuishutumu Serikali ya Dr
Mrisho Kikwete,kwamba,Serikali kupitia wizara ya elimu haijafanya chochote
katika kukuza elimu nchini,zaidi ya kuwalimbikizia kodi kila kukichakitu kinachosababisha kushindwa kutoa misaada kwa shule nyingine ,hasa za serikali ambazo hazina madawati, na vitabu,na kwamba hali ikiendelea hivyo
baada ya miaka 5 kuanzia sasa elimu itakuwa taabani kuwahi kutokea na kutakuwa hakuna elimu katika shule za serikali
ambazo wanaosoma ni wa toto wa wakulima na masikini, alisema Anna Bayi ,
Hata hivyo madai ya
Anna Bayi yamepingwa na wadau mbalimbali walio-ongea na Mtazamomedia,nakuitetea
serikali iliyopo madarakani, kwamba, inafanya kila jitihada mbalimbali kuakikisha elimu inapanda na
kuboreshwa ,Mhe Rais Kikwete ametoa agizo kwa kila shule za Serikali nchi nzima ifikapo desemba 30 /2014 ziwe zina-maabara, hili ni
agizo a lilotoa mhe Rais kwa manisipaa zote nchini ,na hili agizo limeisha anza
kutekelezwa na manisipaa nyingi nchini,ikiwapo manisipaa ya kinondoni,ambayo
hivi karibuni iliitisha kiakao na kukutana na wadau mbalimbali wa elimu
kujadili namna ya kupata pesa zitakazo wezesha kujengwa kwa maabara ili
wanafunzi waweze kupata elimu kwa njia ya nadharia na vitendo,kitu ambacho ni
hatua muhimu sana katika kufikia upatikanaji wa elimu bora nchini.
Imezuka tabia kwa
baadhi ya watu na taasisi mbalimbali kubeza kila kitu kinachofanywa na
Serikali,ama kiwe kizuli au kinakasoro,Serikali ya awamu ya4 imefanya mambo
mengi mazuli rakini baadhi ya watu kwa makusudi wamekuwa wanabeza kama vile
hawaoni alisema Mzee Athumani wa Magomeni Usalama,
