Marcos Maidana kulia akipokea ngumi ya jebu kutoka kwa Floyd Mayweather
IMEANDALIWA NA BERNARD KWA NIABA YA MTANDAO
.
Pambano la karne la
Ngumi kugombea mikanda ya uzito WBA –WBC na SUPERWELTER WEIGHT TITLE kufanyika
May 15/2015 kati ya wapinzani wa kubwa katika uzani huo, kati ya Bingwa wa Dunia,Floyd Mayweather,na Manny Pacguiao
imefahamika jumamosi ,baada ya kumalizika pambano la kugombea ubingwa huo ,kati
ya Floyd na Marcos Maidana lililofanyika septemba 13 -2014 na majaji wote 3
kumpa ushindi wa points Floyd,pambano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Mgm
Grand Garden ,Arena Las Vegas,mala baada
ya kutangazwa mshindi ,aliulizwa swali na waandishi wa habari kama yuko tayari
sasa kupambana na Mfilipino Pacguiao ,alijibu milango iko wazi kwa kufanyika
kwa pambano hilo ,ambalo linasubiliwa kwa hamu kubwa sana na wapenzi wa
masumbwi Duniani.
Simuogopi wala
kukwepa kupigana na Pacguiao tayari nimeongea na timu yangu nzima kuruhusu
kufanyika kwa pambano hilo alisema Floyd alipokuwa akijibu maswali aliyoulizwa
na waaandishi wa habari.
Iwapo hilo pambano
litafanikiwa kufanyika ,wadau mbalimbali wa mchezo wa ndodi ,wamelitabilia
kuvunja rekodi ya dunia litakuwa The super Ghost,na kila bondia litamuingizia
kitita kikubwa cha dola,na litakuwa pambano lililodhaminiwa kwa pesa nyingi
kuliko pambano lolote Duniani
