Mkuu wa mkoa
wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda (kushoto )akimkabidhi zawadi ya Kikombe
Mshindi wa Jumla wa Kombe la Mkuu wa majeshi CDF TROPHY mpiga Golf ambaye ni
Mkuu wa majeshi Mstaafu Jenerali George Watara mara baada ya mashindano katika
Uwanja wa Golf Lugalo Jijini Dar es Salaam jana Septemba 24 .
(Picha na Luteni
Selemani Semunyu) .
Mshindi
wa Jumla wa mashindano ya CDF Trophy 2016 Mkuu wa majeshi mstaafu George
Waitara (wa kwanza kulia)akipokea Mfano wa Tiketi ya Ndege aliyopewa baada ya
kushinda Wapili kulia ni Mnadhimu mkuu wa jeshi Luteni Jenerali
Venance Mabeyo,watatu Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda
na Wakwanza kushoto ni mwenyekiti wa Lugalo Golf Club Brig Gen Michael Luwongo.
Mshindi
wa Jumla wa mashindano ya CDF Trophy 2016 Mkuu wa majeshi Mstaafu George
Waitara (wa kwanza kulia)akipiga mpira wakati wa mashindano hayo katika uwanja wa Golf Lugalo Dar es
Salaam wakwanza kushoto ni katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi Mh Job Masima
Watoto
Junior walioshiriki mashindano ya Kombe la mkuu wa majeshi CDF Trophy wakiwa
katika harakati za mchezo huo katika mashindano yaliyofanyika uwanja wa Golf
Lugalo jana Jumamosi Septemba 24 Jijini
Dar es Salaam.
Baadhi
ya Watoto (Junior) wasichana walioshiriki mashindano ya Kombe la mkuu wa
majeshi CDF Trophy wakiwa katika harakati za mchezo huo katika mashindano
yaliyofanyika uwanja wa Golf Lugalo jana Jumamosi Septemba 24 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Watoto( Junior) walioshiriki mashindano ya Kombe la mkuu wa majeshi CDF
Trophy wakiwa katika harakati za mchezo huo katika mashindano yaliyofanyika
uwanja wa Golf Lugalo jana Jumamosi Septemba 24
Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wachezaji Wanawake( Ladies) walioshiriki mashindano
ya Kombe la mkuu wa majeshi CDF Trophy wakiwa katika harakati za mchezo huo katika
mashindano yaliyofanyika uwanja wa Golf Lugalo jana Jumamosi Septemba 24 Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Luteni
Selemani Semunyu).
.........................................................................................
Na Luteni Selemani Semunyu ,JWTZ
Mpiga Golf na Mkuu wa majeshi Mstaafu George Waitara
ameibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya CDF Trophy yaliyomalizika Jumamosi Septemba 24 katika uwanja wa Golf Lugalo
Jijini Dar es Salaam baada ya kuwashinda wapiga Golf Zaidi ya 100 walioshiriki
mashindano hayo.
Mkuu huyo wa majeshi Mstaafu anayetokea Klabu ya Lugalo aliibuka mshindi baada ya kupata Net ya 70 baada ya kupata
mikwaju ya Jumla 88 huku kiwango cha uchezaji kikiwa ni 18 na hivyo mbali na
kikombe alikabidhiwa Tiketi ya kwenda na kurudi Abu dhabi.
Akikabidhi zawadi hiyo mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Paul Makonda aliyekuwa Mgeni Rasmi
aliahidi kuhakikisha ushirikiano na jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania
JWTZ unaendelezwa hasa katika kuendeleza michezo mbalimbali ikiwemo Golf.
Pia aliomba JWTZ katika hatua za kuhamia Dodoma na ujenzi wa
Uwanja mpya wa Golf usibadili matumizi ya uwanja wa Awali wa Golf Lugalo ili
kutoa nafasi ya kuendeleza mchezo huo lakini kuonyesha historia ya mchezo huo
nchini kwa maana ya uwanja ulikoanzia.
Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Golf ya Lugalo Brigedia jenerali
Michael Luwongo alisema wameshafanikiwa kupata hekta 250 Kilometa nane toka
Dododoma mjini na Kilometa Mbili toka Barabarani sehemu ambayo wanatarajia
kujenga uwanja wa kisasa Zaidi ya wa Awali wa Lugalo.
“Tumepata sehemu hivyo katika kutekeleza Agizo la kuhamia
Dododoma tunaenda nalo sambamba na tutajenga uwanja wa Kisasa pia mwaka huu
tunafikisha miaka 10 ya Klabu pia tutaandaa mashindano mazuri kuenzi waasisi wa
Klabu hiyo” Alisema Brigedia Jenerali Luwongo .
Katika hafla ya Utoaji wa Zawadi na Ufungaji wa Mashindano
hayo Mkuu wa Wa majeshi ya Ulinzi
Jenerali Davis Mwamunyange aliwakilishwa na Mnadhimu mkuu wa jeshi Luteni
Jenerali Venance Mabeyo .
Katika Makundi mengine Daraja a mshindi S Brown aliyepata
Net ya 70,akifuatiwa na Dk Mndolwa aliyepata net ya 73, Daraja B kanali kalino
Kondwani aliibuka na ushindi kwa net 70 akifuatiwa na Telens Mwakalukwa
aliepata net 72.
Kwa upande wa Daraja
C Alfred Kinswaga aliibuka na ushindi
kwa net 70 akifuatiwa na Kapten Amanji Mandengule kwa Net ya 77 huku Senior
akishinda Charles Sanga kwa Net ya 75 akifuatiwa na Salvatory Rwabizi kwa net
ya 76.
Wanawake akishinda Clelensia Kavula kwa net 70 wakati
wachezaji wasaidizi mshindi ni Richard Tweve kwa net ya 69 akifuatiwa na Reuben
Shaban kwa Net ya 70 huku mwanamke pekee kwa kundi hilo Rehema Nyenza akishinda
kwa Net ya 87.







0 Comments