Mshindi
wa Kwanza wea Division A wa Mashindano
ya Wazi ya Arusha Open Kapten Shaban
Kibuna akiwa katika harakati za mchezo huo katika mashindano yaliyomalizika
Jumapili Oktoba 16 Jijini Arusha.
Mshindi
wa Kwanza wa kundi la Wadogo Junior wa
Mashindano ya Wazi ya Arusha Open Almadious Simon akiwa katika harakati
za mchezo huo katika mashindano yaliyomalizika Jumapili Oktoba 16 Jijini Arusha
.
Mchezaji wa Golf wa
Timu ya JWTZ ya Lugalo Nicholous Chitanda akiwa katika harakati za Mashindano
ya Wazi ya Arusha Open katika mashindano yaliyomalizika Jumapili Oktoba 16
Jijini Arusha .(Picha na Luteni Selemani Semunyu).
......................................................................................................................
Na Luteni Selemani Semunyu
JWTZ
Mashindano ya Wazi ya Golf Arusha open yamemalizika jijini
Arusha Oktoba 16 huku Timu ya Golf ya Jeshi la Ulinzi la wananchi wa
Tanzania ya Lugalo ikifanya vizuri kwa kunyakua ushindi katika makundi kwa asilimia 53 huku
ushindi wa Jumla ukichukuliwa na Mchezaji kutoka klabu ya Kilimanjaro.
Mpiga golf wa Timu ya Kilimanjaro issack Wanyeche akiibuka
mshindi wa jumla wa mashindano hayo yaliyokuwa yakishindanishwa kwa mtindo wa
Mikwaju ya Jumla Net kwenye makundi na Gross kwa ushindi wa Jumla.
Katika Division A Mshindi
ni kapteni Shaaban Kibuna kutoka Klabu ya Liugalo akifuatiwa na Richard Mtweve
naye wa Lugalo ambaye walifungana kwa Mikwaju ya Jumla 145 kila mmoja lakini
kutokana na kapteni kibuna kucheza vizuri siku ya mwisho akamshinda Mtweve
kutokana na kucheza net ya 70 kwa 75 wakatik siku ya kwanza ilikuwa 75 kwa 70
ya Mtweve.
Kundi B ambalo Timu
ya Lugalo haikuingiza mchezaji katika kundi hilol imechukuliwa na N Matsouka wa Arusha aliyepata mikwaju ya
Jumla 143 akifuatiwa na mshindi wa pili
ni Musadiq Versi aliyepiga mikwaju ya Jumla 147.
Divisheni C Mshindi
ni Talib Chagani aliyepiga Mikwaju ya Jumla 148 akifuatiwa na kapteni Amanzi Mandengule wa lugalo
aliyepiga mikwaju ya jumla 149.
Kwa upande wa Kundi la wadogo Junior mshindi ni Almadiuos
Simon kutoka Klabu ya Jeshi ya Lugalo kwa kupiga Mikwaju ya Jumla 131 huku mshindi wa Siku ya kwanza ni Salim Sharif
aliyepata Net ya 70 na Mshindi wa Siku ya Pili ni Clemence Mutavangu wa
Lugalo aliyepiga Net ya 69.
Kwa Upande wake Nahodha wa Klabu ya jeshi ya Lugalo ambaye
ni Mshindi wa Divisheni
A kapten Shaban
Kibuna amesema wamefanya vizuri kutokana kuingiza wachezaji 14 na
kunyakua nafasi tano ukilinganisha na Arusha waliongiza wachezaji zaidi
ya 50 na TPC walioingiza wachezaji 17 na kutoka bila ushindi.
Alisema kinachofuata sasa ni klabu yake kujiandaa na mashindano yaliyoko
mbele yao ya Oktoba 22 Mwaka huu lakini pia wanatarajiwa kuwa na mshindano ya Waitara Trophy na Miaka 10 ya Klabu mwezi Desemba.


