
Na Is-haka Omar, Zanzibar.
...........................
CHAMA
Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka Wanachama wa Chama hicho na
wananchi kwa ujumla kupuuza na kudharau propaganda zinazotolewa na
baadhi ya Vyama vya Upinzani kwa lengo la kuwapotezea muda wananchi.
Hayo
yalisemwa kwa nyakati tafauti na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai
ali Vuai huko Mkoa wa Kusini Pemba, alipokutana na Kuzungumza na Kamati
ya Siasa ya Mkoa huo pamoja na Wanachama wa CCM Tawi la Vitongoji.
Naibu
Katibu Mkuu alisema Wapinzani wanajua fika kuwa hakuna na wala
hakutakua na Uchaguzi Mkuu mwengine Tanzania bara na Zanzibar hadi
mwaka 2020, na wanachokifanya kwa sasa ni kuendeleza siasa zisizokuwa na
maslahi kwa familia maskini za Wazanzibar .
Alieleza
kwamba wanasiasa wanatakiwa kuwa wazalendo na kusoma alama za nyakati
kwa kufanya siasa zinazowahamasisha wananchi wafanye kazi kwa bidii za
kujiletea maendeleo badala ya kuwapotosha.
“Wana
CCM na wananchi kwa ujumla tumemaliza Uchaguzi wa marudio na kwa sasa
tufanye kazi za kujiongezea kipato na kujiletea maendeleo huku
tukisubiri kufanya siasa katika uchaguzi ujao na sio wakati huu.
Pia
tunajua kuwa wapinzani hasa CUF kwa upande wa Zanzibar tumewathibiti
kila upande na hawana pakutokea ndio maana wanaangaika kila kona ya
dunia kuomba msaada ili kurudi katika ushindani wa kisiasa jambo ambalo
haliwezekani kwa sasa .”, alisema Vuai.
Nd.
Vuai aliwaomba Wanachama wa Chama hicho kutumia Uchaguzi wa ndani
unaotarajiwa kufanyika 2017, kwa kupata Viongozi imara wa CCM wenye
uwezo wa kuendeleza Ushindi wa Chama katika Uchaguzi ujao.
Naibu
Katibu Mkuu huyo aliwapongeza Wabunge, Wawakilishi na Madiwani wa Chama
Cha Mapinduzi Pemba kwa kua karibu na Wananchi katika utekelezaji wa
Ilani ya uchaguzi kwa kiasi kikubwa ndani ya kipindi kidogo cha Uongozi
wao.
Aidha
Vuai aliridhishwa ukomavu wa kisiasa uliopo kwa wafuasi wa chama hicho
Pemba kwa kuendelea kuwa na Ujasiri wa kuimarisha CCM licha ya
kukabiliwa na Changamoto mbali mbali zikiwemo kuharibiwa Mali zao na
kufanyiwa fujo za mara kwa mara.
Aliahidi
kwa kusema kuwa CCM itaendelea kuwa karibu na wafuasi wake hasa waliopo
Pemba ili kujenga mahusiano mema na ukaribu wa uimarisha Chama hicho
kwa lengo la kujenga ngome ya ushindi kisiwani humo.
Alitoa
wito kwa Vyomb vya Dola kuendelea kuwa macho na Wanasiasa wenye nia za
kufanya vitendo vya uovu kwa kupanga na kutekeleza njama za kuwagawa
wananchi kwa kutumia njia za Dini kupitia nyumba za ibada jambo ambalo
likiachwa linaloweza kuhatarisha amani ya nchi wakati wowote.
Nd.
Vuai alitoa ufafanuzi huo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa
Wanachama wa Chama hicho aliokutana nao katika ziara zake zinazoendea
Unguja na Pemba za kukutana na Viongozi na wanachama wa CCM.
Pamoja
na hayo aliiomba Serikali kutowafumbia macho watu wanaovunja Katiba na
Sheria za nchi kwa makusudi kwa kutumia mbinu chafu na hadaa kwa jamii.