Meneja
Mradi wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi cha Madimba, Sultan Pwaga ( wa pili kutoka kulia mbele) akimwongoza Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa ( wa tatu kutoka kulia
mbele) kwenye ziara ya kukagua kituo hicho ili kujionea shughuli zake.
Meneja
Mradi wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi cha Madimba, Sultan Pwaga akielezea shughuli za kiwanda hicho mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (hayupo pichani)
Meneja
Mradi wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi cha Madimba, Sultan Pwaga (kulia) akifafanua jambo kwa
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (kushoto)
katika ziara hiyo.
Eneo
la mwanzo la bomba la kusafirisha gesi kuelekea Dar es Salaam kupitia Mtwara, Lindi na Pwani kama linavyoonekana
pichani.
Sehemu
ya kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba kama inayoonekana pichani.
Meneja
Mradi wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi cha Madimba, Sultan Pwaga (kushoto) akitoa maelezo hukusu
mikakati inayofanywa na kiwanda hicho katika kuhakikisha kuwa gesi ya uhakika
inapatikana kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin
Ntalikwa (kulia)
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa akisaini kitabu cha
wageni mara baada ya kuwasili katika chumba cha kuongozea mitambo (control
room) katika kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (kushoto)
akifuatilia maelezo ya namna ya
uendeshaji wa mitambo ya kuchakata gesi ya Madimba yaliyokuwa yanatolewa na Stanslaus Malya (hayupo pichani)
Mtaalam
kutoka kiwanda cha kuchakata gesi cha
Madimba, Stanslaus Malya akionyesha uongozwaji wa mitambo unavyofanywa katika
kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa (waliokaa mbele
katikati) na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC)
Kapuulya Msomba ( kushoto waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na
wataalam wa kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba na wataalam kutoka Wizara ya
Nishati na Madini, Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) na TPDC.









