Naibu Waziri
wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Mhe. Chum Kombo Khamis akifungua pazia
kuashiria ufunguzi wa Makumbusho ya watu wa zamani yaliopo Kuumbi Jambiani,
Mkoa Kusini Unguja.
Baadhi ya
wananchi na wafanyakazi wa Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale walioshiriki
ufunguzi wa Makumbusho ya Watu wa zamani Kuumbi wakifuatilia sherehe hizo.
Mtafiti wa
Chuo Kikuu cha Dar es salaam Professa Felix Chami kwanza (kulia) akitoa maelezo
juu ya utafiti uliofanywa na kupelekea kuanzishwa kwa makumbusho ya Kuumbi Jambiani.
Mkuu wa
Divisheni ya Mambo ya Kale Zanzibar Abdallah Khamis Ali akitoa maelezo kwa
Naibu Waziri wa Habari, Utalii Utamaduni na Michezo Chum Kombo Khamis wa kwanza
(kushoto) wakati wa ufunguzi wa makumbusho ya Kuumbi.
Naibu Waziri
wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Chum Kombo Khamis akizungumza na
wananchi na wafanyakazi wa Idara ya Makumbusho wakati wa ufunguzi wa Makumbusho
ya Kuumbi, Jambiani Mkoa Kusini Unguja.
Picha na
Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.




