Random Posts

MASAUNI AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUIMARISHA ULINZI MIPAKANI

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Hamad Masauni, (mwenye tisheti nyekundu) akielekea kutizama mpaka wa Tarekea  wilayani Rombo ili kujionea changamoto zinazotokana na mipaka hiyo pamoja na kutoa maagizo kwa viongozi wanaohusika kuimarisha ulinzi wa mpaka huo ili kukabiliana na upitishaji wa bidhaa za magendo pamoja na wahamiaji haramu ambao wamekua wakiinia nchini bila vibali. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimaanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi Wilbrod Muutafungwa akifatiwa na Kamishna wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro, Mwanguku, na wan ne kutokea kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Rombo Agnes Hokororo alieambatana na Naibu Waziri huyo kuangalia mipaka hiyo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimajaro alipotembela mpaka wa Tarakea wilayani Rombo Naibu waziri Masauni amesema kuwa licha ya changamoto zinazojitokeza katika mipaka yote miwili ni lazima kuendelea kuimarisha ulinzi kwenye mipaka hiyo na kudhibiti njia zote zisizo rasmi zinazotumiwa na wahamiaji haramu pamoja na wafanyabiashara za magendo.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun akionyeshwa Mpaka katika picha unaotenganisha Tanzania na Kenya ulioko Holili wilayani Rombo alipofanya zaiara ya siku moja ya kikazi kuangalia mipaka hiyo na kutoa maelekezo kwa wahusika wa kulinda mipaka hiyo namna ya kuweza kukabilina na changamoto zilizopo katika mpaka huo.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun akipewa maelezo na Afisa Mipaka Holili Michel Amo, juu ya jiwe  linaloonyesha mpaka wa Tanzania na Kenya lililopo katika mpaka wa Holili ambalo limekua likisogezwa na watu wasiojulikana hivyo kuharibu alama za mipaka. Naibu waziri Masauni amesema kuwa licha ya changamoto zinazojitokeza katika mipaka yote miwili ni lazima kuendelea kuimarisha ulinzi kwenye mipaka hiyo na kudhibiti njia zote zisizo rasmi zinazotumiwa na wahamiaji haramu pamoja na wafanyabiashara za magendo.
.....................................................................................................

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni avitaka vyombo vya ulinzi na usalama nchini kuzidi kuimarisha ulinzi katika mipaka ili kushirikiana na Serikali katika mpango wa kupambana na uhalifu  nchini.

Masauni aliyasema hayo leo wakati alipofanya ziara katika mipaka ya Tarakea  na Holili iliyopo mkoani Kilimanjaro ili kujione changamoto zinazojitokeza katika mipaka hiyo ambapo tarifa zinaonyesha kwamba kuna njia zisizo rasmi zaidi ya 265 zinazotumiwa kuptisha bidhaa za magendo na wahamiaji haramu
Katika ziara hiyo Naibu Waziri Masauni alivitaka vyombo vyote vya ulinzi na Usalama nchini kuhakikisha vinaashirikiana kila mtu kwa nafasi yake ili kupambana na uhalifu wa kupitisha bidhaa za magendo zinazopitishwa katika mipaka hiyo na kuikosehsa serikali mapato.

Masauni alisema kuwa Serikali ya awamu ya Tano ina dhamira ya kupeleka nchi katika uchumi wa kati hivyo ni lazima kwa vyombo hivyo kudhibiti biashara zote zinazopita kimagendo mipakani humo lakini pia kuepuka rushwa ili kupiga hatua mbele za kimaendeleo.

Pamoja na kuwapo kwa changamoto ya nguvu kazi na vitendea kazi serikali itahakikisha inaaandaa maofisa wa kutosha mipakani humo ili kuongeza nguvu kazi wakati wa operesheni zao na doria wakati wote.

Aidha Masauni ametoa rai kwa watumishi wa vyombo hivyo kujiepusha na tabia ya kushirikiana au kuwaficha wafanyabiaashara wanao jihusishaa na biashara ya maagendo.


Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimaanjaro Kamishna Msaidizi Mwqaandanizi Wilbrod Muutafungwa almueleza naibu Waziri huyo licha ya changamoto zilizopo wanaendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya mipaka kwa kufanya doria mara kwa mara licha ya kwamba wafanyabiashara hao wa bidhaa za magendo kutumia mbinu mbalimbali kukwepa ushuru lakini Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeweza kuwatia mbaroni.