Random Posts

MASAUNI ALITAKA JESHI LA MAGEREZA KUTEKA SOKO NDANI YA NCHI

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alipowasili katika Gereza Kuu la Karanga, Mkoani Kilimanjaro wakati alipotembelea  kiwanda cha viatu kilichopo gerezani haapo ili kujionea uzalishaji wa bidhaa mbalimbali hasa viatu. Naibu Waziri huyo amelitaka Jeshi hilo kuzidi kuboresha bidhaa za viatu hivyo ili kujipatia soko kubwa ndanni ya nchi na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanattumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni  akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Karanga, Kamishna Msaaidizi Mkwiche  mkoani Kilimanjaro wakati alipofanya ziara katikaa Kiwanda cha viatu kilichopo katika gereza hilo ili kujionea  uzalishaji wa bidhaa za viatu ambavyo Rais Magufuli alitaka majeshi yote nchini kutumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akisikiliza maelezo kuhusu uzalishaji wa viatu katika kIwanda cha Gereza la Karanga kutoka kwa Fundi Mkuu wa Kiwanda hicho Ali Jambaraga wakati alipofanya ziara yake kwenda kujionea uzalishaji wa bidhaa mbalimbali lakini pia  ametaka  wazidi kuzalisha bidhaa bora zaidi ili kuteka soko la ndani na je ya nchi ikiwa ni pamoja na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini kutumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akijionea  kiatu aina ya Safari buti kinachozalishwa na Kiwanda cha Karanga kilichopo Mkoani Kilimanjaro wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja kiwandani katika Mkoa huo. Masauni amesisitiza kiwanda hicho kuzalisha bidhaa bora zaidi ili kuteka soko kubwa zaidi pamoja na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanatumia viatu vinavyozalishwa na Jeshi hilo. Kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho Mrakibu Msaidizi, Michel Minja na kushoto ni Ali Jambaraga Fundi Mkuu.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akiangalia kiatu kilichokuwa tayari kuvaliwa kilichotengenezwa katika kiwanda  cha Karanga kilichopo Gereza Kuu la Karaga mkoani Kilimanjaro. Naibu Waziri huyo amesisitiza Jeshi hilo kuzidi kutengeneza bidhaa bora zaidi za viatu ili kuhakikisha wanapata soko kubwa ndani nan je ya nchi., kulia ni Kamishan Msaidizi Mwandamizi  wa Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa aliye aambatana nae kwenye ziara hiyo.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun (aliyevaa koti) akitoa maelekezo kwa Wakuu wa Gereza la Karanga na kiwanda cha Viatu kilichopo gerezani hapo. Masauni amelitaka jeshi hilo kuzidi kutoa bidhaa bora ili kuendelea kuteka soko kubwa ndani nan je ya nchi.
.................................................................................................
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun aagiza Jeshi la Magereza kuzidi kuboresha viatu vinavyotengenezwa na kiwanda chao ili kujipatia soko kubwa ndani ya nchi na nje.

Hayo aliyasema jana kwa wakuu wa Gereza la karanga na viongozi wa kiwanda hicho alipofanya ziara yake ya siku moja katika kiwanda cha viatu kilichopo katika gereza hilo, mkoani Kilimanjaro

Aidha, Naibu Waziri huyo alisisistiza Jeshi hilo kutekeleza agizo la Rais John Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanatumia viatu vinavyozalishwa na Jeshi la Magereza, hivyo ni muhimu kuendelea kuzalisha bidhaa zilizo bora zaidi

Haiingii akilini maofisa wa majeshi mbalimbali nchini kuagiza viatu nje ya nchi wakati viwanda vya ndani vinauwezo wa kuzalisha viatu bora zaidi vinavyodumu kwa muda mrefu kuliko vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi, alisema Masauni.

Masauni alisema kwamba dhamira ya Serikali ya awamu ya tano ya kuipeleka nchi katika uchumi wa kati hivyo Jeshi la Magerezaa kupitia kiwanda chake na miradi mingine mingi halina budi kuendelea kuzidisha kuzalisha viatu bora vitakavyo kidhi kiwango cha uhitaji na soko ili kukuza uchumi wao na Serikali kwa ujumla.

Aidha, katika ziara yake, Naibu Waziri Masauni amesisitiza kuwa ni muhimu Jeshi hilo kufanya miradi mingi kwa ustadi mkubwa ili kujipatia psa zitakazosaidia kujiendesha wao kama jeshi na mashirika mengine yanayounga mkono miradi yao hivyo kutotegemea ruzuku kutoka serikalini.

 Waziri huyo alilipongeza Jeshi hilo kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora kulinganisha na nyingine zinazoingizwa nchi, hivyo amesisitiza kuzidi kutengeneza viatu bora zaidi ili kuwa na uwanja mpana wa soko la ndani nan je ya nchi.