Random Posts

ALLIANCE YAIZAMISHA SINGIDA UNITED BAO 1-0 LIGI DARAJA LA KWANZA,MATOKEO MENGINE YAPO HAPA TAZAMA.

Na.Alex Mathias.

Timu ya Alliance imeng'ara katika uwanja wake wa nyumbani wa CCM Kirumba baada ya kuwatandika vijana wa kocha Minziro,Singida United goli 1-0 mchezo wa Ligi Daraja la kwanza ukiwa ni wakundi C na kujitupa hadi nafasi ya kwanza huu na kumaliza mzunguko wa kwanza.

Kabla ya kukutana Singinda United walikuwa wanaongoza Ligi kwa pointi 16 huku Alliance walikuwa na pointi 14 na kwa matokeo vijana wa jiji la Mwanza wamefikisha jumla ya pointi 17 katika msimamo wa kundi hilo.

Kiujumla mchezo ulikuwa mgumu kwa kila timu huku Singida wakiongozwa na wachezaji wakongwe waliowahi kuwika katika Ligi Kuu Tanzania Nizar Khalfa pamoja na mdogo wake na Rashid Gumbo wakati Alliance wanatumia vijana wadogo na wengine wapo katika kikosi cha Serengeti boys chini ya umri wa miaka 17.

Kundi hilo ndilo linalotabiriwa kuwa ngumu kwa timu hizo mbili kuchuana vikali ili kutafuta nafasi ya kupanda Ligi Msimu ujao kwani kwenye msimamo unasomeka Alliance 17,Singida 16,Rhino 13,Panone 6 na Polisi Dodoma 6.

TAZAMA MATOKEO MENGINE YA DARAJA LA KWANZA:
.Rhino 2-0 Panone

.Kiluvya 1-0 Friends

.Ashanti 1-1 Lipuli

.Transit Camp 2-2 Milambo

.Burkina Faso 0-1 Changanyikeni

.Mvuvuma 1-0 Polisi Mara

.Polisi Dodoma 0-1 Mgambo.

Post a Comment

0 Comments