Random Posts

VIWANJA SITA VITANI KESHO LIGI KUU TANZANIA BARA,MACHO YA WENGI NI MJINI MBEYA.

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.

.............................................

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajia kuendelea kesho viwanja Sita timu kutafuta alama tatu muhimu ili kujiweka katika nafasi nzuri wadau wengi pamoja na wapenda soka watakuwa wanaangalia viwanja vya Uhuru jijini Dar es salam pamoja Sokoine mjini Mbeya bila kusahau uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Katika jiji la Dar es salaam kutakuwa na wenyeji wa Dar timu ya African Lyon itapambana na Simba kwenye Uwanja wa Uhuru, mchezo Na. 144 wakati Mbao FC itakuwa mwenyeji wa Azam  kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza  mchezo Na. 116.

Mkoani Mtwara kutakuwa na vita ya wenyeji Ndanda FC watakowaalika wapiga debe toka Shinyanga timu ya Stand United ambayo imetoka kujiruhiwa na Mnyama Simba kwa kufungwa goli 1-0  mchezo Na 117 huku Mjini Mbeya kutakuwa na pambano la kukata na shoka wenyeji Tanzania Prisons itacheza na mabingwa watetezi Yanga waliojeruhiwa na Mbeya City kwa kuchezea kichapo cha magoli 2-1  kwenye Uwanja wa Sokoine mchezo Na. 118.

Baada ya kupata ushindi mjini Mwanza dhidi ya Mbao FC Kagera Sugar watacheza na Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba mchezo  Na. 119 wakati wachovu wa Ligi timu ya wanajeshi  JKT Ruvu itawaalika wachovu wenzao toka Mwanza Toto African ‘Wana-kisha Mapanda’ kwenye uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani  mchezo Na. 120.


Hata hivyo Ligi hiyo itaendelea tena Siku ya  Jumatatu kwa michezo miwili , Mtibwa Sugar itawakaribisha wababe wa Yanga kutoka Mbeya timu ya   Mbeya City kwenye uwanja wa Manungu uliopo mkoani Morogoro mchezo Na. 113na Mwadui FC baada ya kupata kichapo kwenye uwanja wao dhidi ya Mtibwa Sugar watakuwa nyumbani tena kucheza na vijana wa Kally Ongala timu ya Majimaji inayosuwasua kwenye msimamo kwenye Uwanja wa Mwadui Complex Shinyanga mchezo  Na. 115.

Post a Comment

0 Comments