Kaimu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Naibu Balozi
Msafiri Marwa akizungumza na Wataalam wa Kujitolea kutoka Shirika
la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA) (hawapo pichani) katika hafla fupi ya kuwakaribisha Wataalam hao ambao watafanya kazi
katika maeneo mbalimbali nchini kwenye sekta za Elimu, Afya na Maendeleo ya
Jamii, hafla iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo,
Mratibu wa
Wataalam wa Kujitolea kutoka Shirika la Kimataifa la Maendeleo
la Japani (JICA), Bw.
Mada Hideki akifafanua jambo kwa Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais –
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Naibu Balozi Msafiri Marwa (hayupo pichani) katika hafla fupi ya kuwakaribisha Wataalam saba wa kujitolea iliyofanyika
Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.
Kaimu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Naibu Balozi
Msafiri Marwa akimsikiliza Mratibu wa Wataalam wa Kujitolea kutoka Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA), Bw. Mada Hideki katika hafla
fupi ya kuwakaribisha Wataalam saba wa kujitolea
iliyofanyika Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.
Kaimu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Naibu Balozi
Msafiri Marwa akiagana na Wataalam wa Kujitolea kutoka Shirika
la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA) mara baada ya hafla fupi ya kuwakaribisha Wataalam hao ambao
watafanya kazi katika
maeneo mbalimbali nchini kwenye sekta za Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii.
....................................................................................
Serikali ya Tanzania imeihakikishia
Serikali ya Japani kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA)
kuwa itaendelea kutoa ushirikiano kwa nchi hiyo ili kuleta maendeleo endelevu
katika sekta mbalimbali nchini ikiwemo afya, elimu na maendeleo ya jamii.
Hayo yalisemwa na Kaimu Katibu Mkuu , Ofisi ya Rais - Menejimenti ya
Utumishi wa Umma, Naibu Balozi Msafiri
Marwa wakati wa hafla fupi ya kuwakaribisha watalaam saba ( 7) wa kujitolea
kutoka nchini Japani iliyofanyika katika
ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.
Kaimu Katibu Mkuu alisema
Tanzania itaendelea kudumisha
ushirikiano huo na Japani ili kuendelea kunufaika hasa katika suala
zima la kujengewa uwezo katika sekta hizo ambazo pia zimepewa kipaumbele katika Awamu ya Pili ya Mpango wa Serikali wa miaka Mitano (5) wa Maendeleo inayoanza mwaka
2016/17 na kumalizika mwaka 2021/22.
Alisema tangu mwaka 1967
hadi sasa vijana wa Japani 1,542 wameshafika nchini na kufanya kazi za
kujitolea katika maeneo mbalimbali hata katika mazingira magumu.
“Pamoja na kunufaika katika
sekta za elimu, afya na maendeleo ya jamii, ushirikiano huo pia unatupa nafasi
ya kubadilishana uzoefu katika kuelewa tamaduni za nchi hizi mbili,” Naibu
Balozi Marwa alisema.
Kwa upande wake, Mratibu wa Wataalam wa Kujitolea kutoka Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA), Bw. Mada Hideki aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa
ushirikiano ambao imekuwa ikiutoa kwa Serikali yao na hivyo kuwawezesha
wataalam wa kujitolea kuweza kufanya kazi waliyoikusudia.
Wataalam hao ambao wako saba
(7) watafanyakazi ya kujitolea katika sekta ya elimu, afya na maendeleo ya
jamii kwa miaka miwili katika mikoa ya Mwanza, Iringa na Mtwara.




0 Comments