Random Posts

SIMBA KUWAKOSA AJIBU,BANDA NA AME ALI WAKATI PRISONS YASEMA MNYAMA LAZIMA AFE SOKOINE HAPA KESHO.

Na.Alex Mathias.
.....................
Kikosi cha Simba kimetua jijini Mbeya kwa kazi moja kuchukua alama tatu muhimu dhidi ya wenyeji Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Sokoine mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara kufunga pazia la mzunguko wa kwanza.
Akizungumza kutoka Mbeya Meneja wa Simba,Mussa Hassani Mgosi amesema kuwa wanamshukuru Mungu kwa kufika salama tayari kwa mpambano huu wa kesho na mchezo huo utakuwa mgumu ila tumejipanga kupata ushindi na kuchukua alama tatu muhimu na pia tutawakosa wachezaji wetu watu kutokana sababu mbalimbali.

"Ni kweli tutawakosa Ibrahimu Ajibu kafiwa na mtoto wake baada ya Mke wake kujifungua na bahati mbaya mtoto alikufa,Abd Banda pamoja na Ame Ali nao hatukuondoka nao kutokana na sababu mbalimbali na wengine waliobaki tuko nao na kesho tunaingia kwa hasira kubwa mno hii ni baada ya kupokea mchezo wetu na African Lyon"alisema Mgosi

Aidha Mgosi amewaomba mashabiki wa Simba pamoja na wanachama kuendelea kushikamana kwa umoja wao na kuwatoa hofu kuwa kesho wataibuka na ushindi kama kawaida japo ni mechi ngumu kwao licha ya kufungwa wekundu wa msimbazi bado wapo kileleni wakiwa na alama 35.

Kwa upande wa Prisons kupitia msemaji wao Enock Mwanguku,amesema kuwa wanaiheshimu Simba kwa kuwa ni kongwe ila wao wapo tayari kuwafunga na kuweza kuchukua alama tatu kamwe hatuwezi kupoteza mara mbili katika uwanja wetu wa nyumbani.

"Sisi tumejeruhiwa kwa kufungwa na Yanga hivyo tunawaonya Simba wasitengemee mteremko kwa kuja kuchukua alama tatu kiukweli tumejipanga na tutashinda Simba wanatujua tunapokutana nao jasho huwa linawatoka"alisema Mwanguku

Post a Comment

0 Comments