Random Posts

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AKABIDHI BODA BODA 200

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Daqarro wakiendesha Pikipiki kabla ya kuwakabidhi  pikipiki hizo vijana 200  wa Jiji la Arusha.

  Dereva wa Bodaboda Dickson Wilbard akijaribu kuendesha Pikipiki aliyokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo.
 Vijana wa Jiji la Arusha wakiwa na Pikipiki zao walizokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (kushoto) pamoja Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqarro (kulia) wakimkabidhi Mlemavu Mohamed Issa (katikati) pikipiki yake aliyopewa kama msaada.
Hizi ndizo Pikipiki aina ya Toyo walizopatiwa vijana 200 wa Jiji la Arusha.
........................................................................................................................

Nteghenjwa Hosseah – Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo amekabidhi pikipiki 200 kwa vijana wa umoja wa wandesha Boda boda Jiji la Arusha (UBOJA) ikiwa ni mkopo wa masharti nafuu  na usiokuwa na riba utakaowawezesha  vijana wa kudni hili kujiajiri na kuondokana na tatizo la ukosefu wa ajira pamoja na umasikini.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo Mhe Gambo amesema kuwa vijana wengi wamekua wakikabiliwa na tatizo la mtaji hivyo pikipiki hizo zitawasaidia kukuza mitaji yao na kuongeza kipato chao cha kila siku hivyo kujikwamua katika lindi la umasikini.
 Aliongeza kuwa Vijana hao wamekuwa wakipata Pikipikizi hizi kwa gharama kubwa zaidi kutoka kwa wamiliki binafsi ambapo inapaswa kulipa mara mbili ya bei ya Pikipiki ndipo unaweza kumiliki au aendelee kurejesha Fedha siku zote mpaka Pikipiki itakapokufa hivyo kunufaisha watu wachache ilihali wao wakiendelea kuwa na hali duni kimasiha.
 “Nimetambua jitihada zenu katika kujitafutia kipato na nimesikia mahitaji yenu kupitia vikoa vyetu tulivyokutana siku za nyuma na nimeona niaze kutatua Changamoto hii ambayo ndio ilikua kubwa na mengine tunaendelea kuyatafutia ufumbuzi kama Bima kubwa kwa wote na Bima ya Afya kwa wale ambao hawapo kwenye pango huu” alisema Gambo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Boda boda jiji la Arusha (UBOJA)   ameshukuru Uongozi wa Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wadhili waliojitolea kuhakikisha kuwa wanatengeneza fursa za ajira kwa vijana 200 katika jiji la Arusha jambo ambalo litainua masiha ya vijana walio wengi.
 Dereva wa Bodaboda Dickson Wilbard amesema kuwa mchango huo wa Mkuu wa Mkoa na wa thamani sana kwa vijana wa Arusha na utawasaidia vijana wengi kuacha kukaa vijiweni na kujihusisha na vitendo vya uhalifu na badala yake watakua wachapa kazi.
Pikipikzi 200 zimegharimu  Tsh Mil 400 sambamba na  bima kubwa (Comprehensive Insurance) kwa Pikipiki 200 sawa na Tsh Mil 27 na vijana watapaswa kurejesha Tsh 7000 kwa siku 305 sawa na Tsh 2,135,000 na watamilikishwa Pikipiki hizo.

Post a Comment

0 Comments