Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Simba imeendelea kujichimbia
kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya ushindi wa goli
1-0 dhidi ya JKT Ruvu mchezo uliomalizika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Timu ya wanajeshi hao miongoni mwa
timu tatu zilizo kwenye mstari wa kushuka daraja pamoja na Toto African
na Majimaji dakika ya 42 kiungo mahiri Mzamiru Yassin aliwapa furaha mashabiki wa Simba baada ya kufunga goli akiunganisha krosi ya Paschal Athanas.
Kipindi cha pili hakuna timu
iliyoweza kupata goli licha ya kufanya mabadiliko mbalimbali hadi
mwamuzi anamaliza mpira Simba wameibuka na ushindi wa goli 1-0 na ukiwa
mchezo wa pili kwa kocha Bakari Shime kupoteza mechi tangu aichukue timu
hiyo.
Matokeo hayo yanaifanya Simba
kuendelea kutesa kileleni mwa ligi ikifikisha pointi 41, alama nne zaidi
ya wapinzani wao Yanga wenye pointi 38 wakiwa nafasi ya pili.

0 Comments