Random Posts

SIMBA KAMA CHELSEA YALA CHRISTMAS KILELENI

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Simba imeendelea kujichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya ushindi wa goli 1-0 dhidi ya JKT Ruvu mchezo uliomalizika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Timu ya wanajeshi hao miongoni mwa timu tatu zilizo kwenye mstari wa kushuka daraja pamoja na Toto African na Majimaji dakika ya 42 kiungo mahiri Mzamiru Yassin aliwapa furaha mashabiki wa Simba baada ya kufunga goli akiunganisha krosi ya Paschal Athanas.
Kipindi cha pili hakuna timu iliyoweza kupata goli licha ya kufanya mabadiliko mbalimbali hadi mwamuzi anamaliza mpira Simba wameibuka na ushindi wa goli 1-0 na ukiwa mchezo wa pili kwa kocha Bakari Shime kupoteza mechi tangu aichukue timu hiyo.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kuendelea kutesa kileleni mwa ligi ikifikisha pointi 41, alama nne zaidi ya wapinzani wao Yanga wenye pointi 38 wakiwa nafasi ya pili.

Post a Comment

0 Comments