Random Posts

WAZIRI MHAGAMA: KAMILISHENI UKARABATI WA NYUMBA ZA WATUMISHI MWISHO WA MWEZI HUU.



 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akizungumza na viongozi mbalimbali wa Mamlaka ya Ustawishaji wa makao makuu(CDA) Dodoma na mkandarasi kwa pamoja wanasimamia mradi wa ukarabati wa makazi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika eneo la kikuyu mkoani Dodoma.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akiongea jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu kutoka wizara hiyo Issa Nchasi wakati akikagua ujenzi wa makazi ya waziri mkuu Mkoani Dodoma.Nyuma ni moja ya ofisi ambayo imekamilika.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akimskiliza Mhandisi Mhandisi  Joseph Muhamba kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu juu ya maendeleo ya ujenzi wa Makazi ya Mhe.Waziri Mkuu.Wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu kutoka wizara hiyo Issa Nchasi na Mkurugenzi msaidizi wa Idara hiyo  Samwel Mwashambwa.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi  Joseph Muhamba kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu wakati Waziri uyo alipotembelea na kukagua maendeleo ya Ujenzi wa makazi ya  Waziri mkuu eneo la Mlimwa,Dodoma.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akiangalia maendeleo ya ujenzi wa Barabara na Madaraja   katika Ofisi mpya Waziri Mkuu iliyopo eneo la Mlimwa,Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama akikagua  ujenzi wa tanki la kuhifadhi na kupeleka maji katika makazi ya waziri Mkuu eneo la Mlimwa,Dodoma.Tenki hilo lina uwezo wa kuhifadhi lita laki mbili kwa siku.


Picha na Daudi Manongi-MAELEZO.
................................................................................................................

Na Daudi Manongi-MANONGI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama amemwagiza mkandarasi anayesimamia ukarabati wa nyumba watakazo ishi watumishi wake kukabidhi nyumba hizo ifikapo tarehe 28 Mwezi huu.

Ameyasema hayo wakati akikagua ukarabati  wa makazi ya watumishi wake yaliyopo eneo la kikuyu mkoani Dodoma yanayosimamamiwa na Mamlaka ya Ustawishaji wa makao makuu Dodoma(CDA).

“Kama wote mnakumbuka agizo la mheshimiwa Waziri mkuu kwamba kufikia mwezi Februari mwakani Mawaziri wote,Manaibu Waziri,Makatibu wakuu na Manaibu wake pamoja na sehemu ya watumishi wachache wa kila wizara lazima wawe wameshafika Dodoma na leo tupo hapa kuhakikisha miundombinu iko sawa tayari kwa kazi ambayo tunataka kuifanya tukiwa hapa Dodoma,”Alisema Mhe.Mhagama
Aidha amesema kuwa nyumba hizo zimefikia katika hatua nzuri sana na hivyo ikifika februari wataanza kuhamia kama ilivyoagizwa.

Pia Waziri Mhagama amesema kuwa Ujenzi wa makazi ya Waziri Mkuu pia yamefikia hatua nzuri ambapo kwa sasa wanakamilisha uwekwaji wa tenki la maji ambalo litasaidia kuhifadhi lita laki mbili kwa siku kwa ajili ya matumizi  ya kila siku na pia ujenzi wa barabara mbili zinazofika Ofisi ya Waziri Mkuu mkandarasi ameshakamilisha ujenzi wa barabara hizo tayari kwa matumizi.

Mhe.Mhagama amewahakikishia watanzania na Serikali kwa Ujumla kuwa kufikia Mwezi Februari watahamia Dodoma ili kukamilisha agizo la rais wetu wa awamu ya tano na pia kukamilisha ndoto ya mwalimu Nyerere ya kuihamisha Serikali Dodoma.

Post a Comment

0 Comments