Random Posts

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA MGENI RASMI MKUTANO MKUU MAJAJI WANAWAKE TANZANIA

Na:  Frank Shija – MAELEZO

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni katika Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA).
Hayo yamebainishwa katika taarifa iliyotolewa na Katibu wa Chama hicho  Jaji C. W. Makuru leo jijini Dar es Salaam ambapo katika taaarifa hiyo imesema  kuwa mkutano huo utafanyika siku ya jumamosi, tarehe 07/01/2017 katika ukumbi wa PSPF Goldeni Jubilee Tower ghorofa ya nne.
Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa Mkutano huo utatanguliwa na mafunzo ya uandishi wa hukumu na elimu kuhusu mifuko ya jamii.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo mkutano huo unatarajiwa kuudhuriwa na wa wanachama ambao ni Mahakimu na Majaji 200 kutoka pande zote za Tanzania.

Post a Comment

0 Comments