Random Posts

TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA KUFANYIKA FEBRUARI 9 -12 KATIKA UKUMBI WA MJI MKONGWE MJINI ZANZIBAR .

Mkurugenzi wa Tamasha la Sauti za Busara,Yusuph Mahmoud (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika  Hotel ya Golden Tulip ilioko maeneo ya posta mpya jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na maandalizi ya tamasha la Sauti za Busara linalotarajia kufanyika Februari 9 -12 katika Ukumbi wa Mji Mkongwe Mjini Zanzibar (katika), Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Sauti za Busara, Simai Said (kulia) ni Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne – Marie Kaarstad.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Sauti za Busara, Simai Said (katika) akifafanua kuhusiana na  Tamasha la Sauti za Busara linalotarajia kufanyika Februari 9 -12 katika Ukumbi wa Mji Mkongwe Mjini Zanzibar.
Ambapo amesema tamasha limekuwa likitangaza Tanzania pamoja na kuwaweka Waafrika sehemu moja.
“Sauti za Busara limebakiza siku chache kufanyika pale Mji Mkongwe, Zanzibar 9-12/Februari kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa tamasha la Sauti za Busara lenye kauli mbiu ya ‘AfricaUnited’ mwaka huu tamasha litakua na majukwaa matatu yatakayotumiwa na wasanii wote kimataifa/nyumbani”amesema Simai,( kulia ) Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne – Marie Kaarstad, na kushoto Mkurugenzi wa tamasha la Sauti za Busara,Yusuph Mahmoud,
Mkutano ukiendelea
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo
Wadau wakifuatilia kwa makini maandalizi ya tamasha hilo.
Viongozi wa tamasha hilo wakijadiliana jambo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Busara Promotions ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tamasha la Sauti za Busara, Yusuf Mahmoud ‘DJ Yusuf’ akionesha  kitabu  chenye progamu ya tamasha hilo kwa mwaka huu wa 2017 kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo Jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments