ATCL WAHAIDI HUDUMA BORA KWA WANANCHI - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, 13 February 2017

ATCL WAHAIDI HUDUMA BORA KWA WANANCHI

  MKuu wa Mkoa AELEKEZA safari za kikazi kwa watumishi wa serikali  Mkoa wa Mbeya kutumia shirika la Ndege la Taifa(ATCL)
Asema Uwanja wa   Ndege  wa kimataifa wa Songwe  Ukikamilika utakuwa  ni lango  la kuingia Tanzania kwa nchi zote za kusini mwa Afrika
Ameiomba ATCL  watakapoingiza Ndege nyingine kuweka katika Mipango  ya safari  za Mbeya - Malawi- Dar 
 Uongozi wa shirika la Ndege la Taifa( Air Tanzania) umehaidi kuendelea kutoa huduma bora kwa wateja wake nchini kote  ikiwa ni sehemu YA mikakati yake YA kibiashara
Hayo yamesemwa leo na mwenyekiti wa bodi YA ATCL Ndg Emanuel Koroso na Mtendaji Mkuu wa ATCL Eng Ladislaus Matindi walipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla
Wamewashukuru sana wananchi wa Mkoa wa Mbeya na watanzania wote kwa ujumla kwa ushirikiano wanawapa wa kutumia shirika hilo ktk Safari zao na wamewaomba kuendelea kulitumia shirika hilo ambalo limeboresha huduma zake
 Mkuu wa Mkoa amelishukuru shirika la Ndege kwa kuweka Mkoa wa Mbeya ktk Safari zake na kufanya hivyo limepunguza kero ya wananchi kukwama kusafiri kama ilivyokuwa hapo awali

Aidha ameliomba shirika hilo kuweka ktk Mipango yake watakapopata Ndege zingine kutoa huduma kwa nchi za jirani ikiwemo Malawi na zambia kwa kupitia uwanja wa Ndege wa songwe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages