BILIONI 18.KUTUMIKA KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI DAR - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, 14 February 2017

BILIONI 18.KUTUMIKA KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI DAR

 Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangi’ngo akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu mikakati ya Serikali kuhakikisha kuwa changamoto ya upatikanaji wa maji katika  Jiji la Dar es salaam  inapatiwa ufumbuzi wa kudumu mara baada  ya kukamilika kwa miradi ya Ruvu Juu na Chini pamoja na ule wa uchimbaji wa Visima Virefu katika eneo la Kimbiji  vitakavyozalisha maji yatakayotumika katika Jiji la Dar es salaam na Viunga vyake likiwemo eneo la Kigamboni.
 Moja ya mitambo inayotumika kuchimba visima katika eneo la Kimbiji ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali ya Awamu ya Tano kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es salaam na Viunga vyake.
 Moja ya Kisima kilichochimbwa katika eneo la Kimbiji  kama kinavyoonekana,Kisima hicho ni moja ya visima vinavyochimbwa katika eneo hilo hali itakayochochea maendeleo katika Wilaya ya Kigamboni,Temeke na jiji la Dar es salaam kwa ujumla mara baada ya kukamilika kwa mradi  huo na ujenzi miundombinu ya kusafirishia maji hayo.

 Sehemu ya Kisima kama inavyoonekana katika Picha 
 Maji yakitoka kwenye moja ya Kisima Kirefu kilichochimbwa katika eneo la Kimbiji unakotekelezwa mradi mkubwa wa unaolenga kutatua changamoto ya maji katika Jiji la Dar es salaam.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa katika eneo la Kimbiji wakati wa ziara ya kutembelea moja ya miradi mikubwa  ya uchimbaji Visima Virefu  inayotekelezwa na Serikali katika kutatua chanagamoto ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es salaam.
 Moja ya Mitambo inayotumika katika uchimbaji wa Visima Virefu katika eneo la Kimbiji,mradi huo ni moja ya mikakati ya Serikali katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika jiji la Dar es salaam.
 Mtambo unaotumika katika uchimbaji Visima Virefu ukiwa katika eneo la mradi huo.
 Sehemu mojawapo  vinapochimbwa Visima virefu vitakavyosaidia kuondoa chanagamoto ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Jiji la Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangi’ngo  akiwaongoza kuelekea katika moja ya maeneo ya utekelezaji wa mradi huo. wataalamu wa Kampuni ya Serengeti Ltd na ile ya NSPT ya Iran zinazotekeleza mradi wa uchimbaji Visima Virefu katika eneo la Kimbiji 
 Msimamizi wa mradi wa uchimbaji Visima Virefu kutoka wa Kampuni ya Serengeti Ltd Bw. Peter Flahant        akionesha kwa waandishi moja ya mitambo katika eneo la kimbiji na jinsi inavyofanya kazi katika uchimbaji wa visima Virefu.
 Msimamizi wa mradi huo toka kampuni ya Serengeti Ltd Bw.Peter Flahant (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangingo.(kushoto) kulia ni mshauri wa mradi huo Bw. Roland Chombo.
 Msimamizi wa mradi huo toka  Kampuni ya Serengeti Ltd Bw.MehrdadTalik (katikati) akisitiza Jambo kwa Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangingo.(kushoto) wakati wa ziara ya waandishi wa habari kutembelea mradi wa uchimbaji Visima virefu katika eneo la Kimbiji kulia ni mshauri wa mradi huo Bw. Roland Chombo.
 Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangingo akionesha kwa waandishi wa habari hawapo (pichani) eneo unapotekelezwa mradi mkubwa wa uchimbaji Visima Virefu viyakavyozalisha maji yatakayotumika katika Jiji la Dar es salaam.
 Mshauri wa mradi huo Bw. Roland Chombo akisisitiza Jambo kwa Mkurugenzi wa Ufundi na Uendeshaji wa DAWASA Mhandisi Romanus Mwangi’ngo.kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Ltd Bw.Mehrdad Talik.
 Moja ya Mitambo inayotumika katika uchimbaji wa Visima virefu ukiwa katika eneo la mradi.
 Sehemu ya Mitambo inayotumika kuchimba Visima Virefu.
 Mtambo unaotumika kuchoronga Visima Virefu ukiwa katika eneo la Kimbiji unapotekelezwa mradi mkubwa wa uchimbaji visima virefu.
 Tanki linalotumika kuhifadhi maji katika miradi iliyobuniwa na DAWASA katika eneo la mbagala na kuendeshwa na wananchi wenyewe ikiwa ni mkakati wa Mamlaka hiyo kuibua miradi ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es salaam.
 Meneja Uhusiano wa DAWASA Bi Neli Msuya akieleza kwa waandishi wa habari faida za miradi inayoibuliwa na Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na wananchi katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es salaam.
(Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo)

Frank Mvungi-Maelezo.
...................................................
Serikali kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka  Dar es Salaam (DAWASA) inatekeleza mradi wenye thamani ya bilioni 18 unaolenga kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es Salaam.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa ufundi na uendeshaji wa Mamlaka hiyo Bw. Romanus Mwang’ingo wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika eneo la Kimbiji ambako ndipo mradi huo unapotekelezwa .

“Mkandarasi anaendelea na kazi  na ameleta mabomba yote na amechimba visima 15 na vitazalisha maji yatakayotumika katika Jiji la Dar es salaam na mradi unatarajiwa kukamilika machi 2017” Alisisistiza Mwang’ingo.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 85 na utakapokamilika maeneo ya Kigamboni,Temeke,Ilala na Jiji la Dar es Salaam kwa ujumla yatanufaika kwa kupata huduma ya maji.

Kwa upande wa miradi  mingine kama ule wa ujenzi wa bomba kutoka Ruvu juu hadi kimara Mwang’ingo amesema  ulikamilika mwezi oktoba 2016 na uzalishaji wa majaribio unaendelea
Mradi huo wenye thamani ya dola za marekani  milioni 59 ni moja ya mikakati ya Serikali katika kuhakikisha kuwa wakazi wa Jiji la Dar es salaam wanapata huduma ya maji safi na salama. na kuondokana na changamoto hiyo. .
Aidha mradi huo utawezesha kiwango cha maji kufikia lita milioni 196 kwa siku kutoka lita milioni 82 za awali.

Kwa upande wake Bw.Salum  Hamis mkazi wa mbagala amepongeza miradi ya maji inayotekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wananchi kwa kuwa imekuwa chachu ya maendeleo katika maeneo yao.

Aliongeza kuwa miradi hiyo imechochea  kupunguza tatizo la maji   na imewawezesha wananchi kutumia muda mwingi katika shughuli za kiuchumi na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi.

Katika kukabilina na tatizo la miundombinu ya maji taka katika Jiji la Dar es Salaam mamlaka hiyo iko katika mchakato wa kuanza ujenzi wa mtambo mkubwa wa kuchuja maji taka katika  eneo la Jangwani  na kuboresha mfumo wa maji taka katikati ya Jiji.

Mradi mwingine ni ule wa upanuzi wa ruvu chini ambao umekamilika kwa asilimia mia moja na utawezesha upatikanaji wa maji kufikia lita milioni 270 kwa siku kutoka milioni 180 kabla ya mradi huo haujatekelezwa.

Majukumu ya DAWASA  ni kumiliki miundombinu ya maji safi na maji taka kwa niaba ya Serikali, kusimamia utoaji wa huduma ya maji safi na maji taka Dar es salaam, kugharimia,kupanga mipango na kusimamia upanuzi wa huduma na kuishauri Serikali kuhusu masuala ya huduma ya maji safi na maji taka Jijini  Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages