Rais wa chama cha walimu Tanzania ( CWT ),Gracian Mkoba akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Mvomero mhe. Mwl Mohammed Utali kuzindua vitabu vya kiingereza vilivyoandikwa na walimu wa Tanzania walio pata mafunzo ya uandishi wa vitabu (kulia), Mkurugenzi mtendaji wa Pana African Teacher's center kutoka Ghana mwl Peter Mabande
Hafla ya uzinduzi huo ulifanyi kati ofisi ya chama hicho zilizopo kinondoni jijini Dar es Salaam leo jumatatu Februari 27, 2017
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Mvomero mhe. Mwl Mohammed Utali akisoma hotuba yake wakati akizundua vitabu vya kiingereza vilivyoandikwa na walimu wa Tanzania walio pata mafunzo ya uandishi wa vitabu.
Mkurugenzi mtendaji wa Pana African Teacher's center kutoka Ghana mwl Peter Mabande akielezea kuhusina na kusaidia watoto wa Africa katika kujifunza lugha ya kiingereza wakati wa uzinduzi huo.
Walimu wakishuhudia uzinduzi huo wa vitabu.
![]() |
| Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Mvomero mhe. Mwl Mohammed Utali (katikati) pamoja na walimu wa chama hicho wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo wa vitabu. (Picha zote na Philemon Solomon-Fullshangweblog ) ........................................ |
Chama cha walimu Tanzania ( CWT) kwa kushirikiana na shirikisho la Vyama vya walimu Duniani kupitia OFISI ya Afrika kitengo cha kuendeleza walimu kitaaluma (ILAF) Leo kimezindua vitabu vya kiingereza vilivyoandikwa na walimu wa Tanzania walio pata mafunzo ya uandishi wa vitabu.
Akizungumza katika uzinduzi wa vitabuhivyo Rais wa chama cha walimu Tanzania Gracian Mkoba amesema vitabu hivyo vya hadith za kubuni vitasaidia wanafunzi washule za msingi na sekondari katika kujifunza lugha ya kiingereza , na vita gawanywa kwa majaribio katika wilaya ya mvomero vikipata mafanikio vitasambazwa nchi nzima.
Amesema katika mafunzo hayo walimu 36 wamefadika na mafunzo huku walimu watano wakitika Zanzibar na walimu 31 wame toka Tanzania bara, na vitabu vilivyo ingizwa katika mpango huo ni vya walimu 17 kati ya walimu 36 walio hudhuria mafunzo hayo ambavyo vilionekana kukidhi vigezo.
Naye Mkuu wa wilaya ya Mvomero mhe. Mwl Mohammed Utali ameshukuru chama cha walimu kuiteua wilayahiyo katika mradi huo ,na kusema kuwa vitabu hivyo vitasaidia kwa kuwa maeneo mengi ya wilaya hiyo ni ya familia za wafugaji wanao hamahama hivyo kupewa vitabu hivyo kutawasaidia kuinua kiwango cha Elimu.
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Pana African Teacher's center kutoka Ghana mwl Peter Mabande amesema wanameanzisha mpango huo kimataifa ili kusaidia watoto wa Africa katika kujifunza lugha ya kiingereza kutoka na hapo awali walimu hawakulipa umuhimu Mkubwa suala la utunzi wa vitabu , na amekipongeza cha cha walimu Tanzania kuitikia mpangohuo na kuupaumuhimuna has a kukubalikughalimia vitabu hivyo na wao wataendelea kusaidia katika kutoa mafunzo kwa walimu.







0 Comments