Random Posts

MAADHIMISHO YA MAHAFALI YA 35 YA CHUO CHA ARDHI MOROGORO

Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dr. Moses Kusiluka (kushoto) akiongoza maandamano na viongozi wa Chuo cha Ardhi  Morogoro, pamoja na  Mkuu wa Chuo cha Ardhi Tabora, Bwn. Justo Lyamuya, wakati wa maafali ya 35 ya chuo cha Ardhi Morogoro.
Mgeni rasmi  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dr. Moses Kusiluka (kushoto) akitoa hotuba katika maafali ya 35 ya Chuo cha ardhi Morogoro, kushoto kwake ni Bwn. Desderius Kimbe, na anayemfuatia ni Mkuu wa Chuo cha Ardhi  Morogoro; Bwn. Justo Lyamuya.
 Katika picha ya pamoja na wahitimu na baadhi ya wanafunzi, katikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dr. Moses Kusiluka, kushoto kwake ni; Bwn. Desderius Kimbe na kulia kwake ni Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro, Bwn. Justo Lyamuya.
 Mgeni rasmi; Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dr. Moses Kusiluka (kulia) akifuatilia kwa makini maelekezo ya  Mwanafunzi wa Chuo cha Ardhi Morogoro, ambaye alikuwa akionyesha jinsi ya kutumia kifaa cha upimaji Ardhi, wakati wa maafali ya 35 ya chuo cha Ardhi  Morogoro.
Mkuu wa Chuo cha Ardhi  Morogoro, Bwn. Justo Lyamuya (katikati) akitoa maelezo ya kina kuhusu matumizi ya kifaa cha upimaji Ardhi kwa baadhi ya waalikwa wa Maafali ya 35 ya Chuo cha Ardhi  Morogoro.

Na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Post a Comment

0 Comments