Rais wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi, ametuma rambirambi kwa familia
ya marehemu Sir George Kahama aliyefariki dunia Jumapili akiwa katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Rais Malinzi amesema taifa
limepoteza mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika kupigania
maendeleo ya mpira wa miguu baada ya kupigania Uhuru ambao Watanzania
leo wanajivunia amani.
Pamoja na familia ya marehemu,
ndugu, jamaa na marafiki, Rais Malinzi Dkt Magufuli amewapa pole
wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi, akisema ni kielelezo cha kiongozi
aliyetukuka.
“Kabla ya Uhuru Mzee wetu, Mzee
Kahama alikuwa kiongozi shupavunamzalendo, alama ambayo ametuachia sisi
Watanzania leo hii tunajivunia amani,” alisema Rais Malinzi.
Rais Malinzi ambaye katika vikao
vyake vya jana hapa Dar es Salaam, alikuwa akitoa nafasi ya kumkumbuka
Sir George, akisema msiba huo pia ni wa TFF kwa kuwa mmoja wa watoto
wake, Joseph ni Mjumbe wa Mfuko wa Bodi ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu
wa TFF.
Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina.

0 Comments