Random Posts

RAIS DK. MAGUFULI KUWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA (INTERCHANGE) ZA UBUNGO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, anatarajiwa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara za juu (interchange), katika makutano ya Ubungo tarehe 20 Machi, 2017.
 
Aidha Rais wa Benki ya Dunia Mheshimiwa Dkt. Jim Yong Kim anatarajiwa kushiriki katika sherehe hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la interchange ya Ubungo.

Mradi wa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya Ubungo ambao utagharimu takribani shilingi bilioni 188.71 una lengo la kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Morogoro, Nelson Mandela na Sam Nujoma.

Mradi huu ni sehemu ya mradi wa uboreshaji usafiri Jijini Dar es Salaam yaani (Dar es salaam Urban Transport Improvement Project), utakaogharimiwa kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia na mchango wa Serikali ya Tanzania ambao utahusisha pia awamu ya tatu na ya nne ya ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (Bus Rapid Transit- BRT), katika barabara ya Nyerere kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongo la mboto na barabara ya Bagamoyo kutoka katikati ya jiji hadi Tegeta.

Post a Comment

0 Comments