Mhandisi wa maji katika halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Grace Lyimo
akizungumza na wananchi wa kata ya Misugusugu baada ya kukagua miradi
mbalimbali ya maji .
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Diwani wa kata ya Misugusugu Ramadhani Bogas akizungumza na wakazi wa
kata hiyo baada ya ujumbe wa idara ya maji katika halmashauri ya Mji wa
Kibaha kwenda kutembelea mradi wa maji wa Zojosa.
(Picha na Mwamvua
Mwinyi)
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Leonardo Mloe akifungua maji
baada ya kutembelea mradi wa maji ZOJOSA huko kata ya Misugusugu.
(Picha
na Mwamvua Mwinyi)
.......................
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
MHANDISI wa maji katika halmashauri ya Mji wa Kibaha,Grace
Lyimo,amewataka wakazi wa mji huo kulinda na kuitunza miundombinu na
mifumo ya miradi mbalimbali ya maji safi kwani maji ni uhai kwa afya na
maisha yao.
Amesema baadhi ya watu wamekuwa wakiharibu miundombinu hiyo
kwa kuikata ama kupasua kwa makusudi hali inayosababisha uchafuzi wa
mazingira ikiwemo matope na kusababisha hasara .
Akizungumza wakati akiwa kutembelea miradi mbalimbali ya
maji Grace alisema ,miradi mingi inatumia fedha nyingi kutoka bank ya
dunia na mengine serikali kuu hivyo kila mmoja athamini miradi hiyo.
Alieleza kwamba ujumbe wa maadhimisho ya wiki ya 29 ya maji 2017 unaenda sambamba na shughuli zitakazofanywa mjini hapo .
Hata hivyo mhandisi huyo wa maji alisema,walianza
kutembelea kituo cha maji cha jumuiya ya maji Zojosa ,kituo ambacho
kinalisha maji mitaa mitatu ya Zogowale,Jonung’ha na Saeni na kupanda
miti 50.
"Tutakagua pia miradi mbalimbali na viwanda ikiwemo kiwanda
cha ngozi na kiwanda cha viuadudu vya kuzuia mazalia ya mbu ambapo
march 22 tutaadhimisha wiki ya maji kwenye mradi wa maji Saeni huko
Viziwaziwa " alibainisha Grace.
Nae katibu wa kituo cha jumuiya ya maji ZOJOSA, Said Kondo
alisema,mradi huo umefadhiliwa na bank ya dunia kwa gharama ya mil
.109.
Alielezea watumiaji maji hadi sasa ni 2,500 kwa siku wanalisha lita 50,000 na kupampu maji masaa sita.
Kondo alisema walianza na vituo 8 sasa vipo 56 na malengo yao ni kufikia wanachi kwa asilimia 80 na zaidi ya hapo .
"Tunachangamoto ya wateja wetu kutolipa bili kwa wakati lakini tuna zaidi ya mil.3.4 bank kwa sasa " alisema Kondo .
Mgeni rasmi ambae ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Kibaha,Leonard Mloe aliomba mradi huo utunzwe na kusimamia makusanyo.
Uzinduzii wa wiki ya maji duniani umeanza march 16 na kilele chake kitakuwa march 22 .





0 Comments