Random Posts

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC)

JAMHURI YA MUUNGANO WA  TANZANIA WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI


TAARIFA KWA UMMA

UTEUZI WA WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI
WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC)
Kufuatia uteuzi wa Bibi Blandina S.J. Nyoni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) tarehe 25/02/2017.  Mhe. William V. Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 5(2) cha Sheria Na. 2 ya Mwaka 1990, amewateua Wajumbe 7 wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa.

Aidha, uteuzi huu ni wa kipindi cha miaka mitatu (3), kuanzia tarehe 23 Machi, 2017.

 Majina ya wajumbe hao ni kama ifuatavyo:
1. Prof. John M. Lupala
2. Bwn. Gabriel Malata
3. Bi. Mary Mlay
4. Bi. Subira Mchumo
5. Bwn. Ally Hussein Laay
6. Bwn. Pius Maneno
7. Bwn. Kesogukwele Masudi Issa Miraji Msita

Imetolewa na:

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Post a Comment

0 Comments