Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki, Mb (kulia) akiwasili
katika Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni leo wakati wa ziara yake ya kikazi
katika Wilaya hiyo kuzungumza na Watumishi wa Umma. Katikati ni Mkuu wa Wilaya
ya Kinondoni Mhe. Ally S. Happi akimkaribisha Waziri Kairuki, na kushoto ni
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Aron Kagurumjuli
Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally S. Happi akizungumza na watumishi wa umma wa
wilaya ya Kinondoni leo (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Angellah J. Kairuki (Mb) katika
Wilaya hiyo kuzungumza na Watumishi wa Umma, Jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Kinondoni
(hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika wilaya hiyo leo Jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni Bibi. Sixtha Kevin
Komba akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) alipofanya
ziara ya kikazi katika wilaya ya Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam.
Afisa
Utumishi Mwandamizi kutoka Idara ya Ukuzaji Maadili Ofisi ya Rais- Utumishi Bi.
Leyla Mavika akitoa ufafanuzi kuhusu masuala ya maadili katika Utumishi wa Umma
wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika Wilaya ya
Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam.
Mstahiki Meya Manispaa
ya Kinondoni Mhe. Benjamini Sitta (kulia) akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Angellah J. Kairuki (Mb) baada ya kupokea hoja za watumishi wa Umma wa Wilaya
ya Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam. Pichani- Katikati ni Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J.
Kairuki (Mb) na kushoto ni Mkurugenzi
Manispaa ya Kinondoni Bw. Aron Kagurumjuli
Picha
na:
Genofeva Matemu - MAELEZO
.....................................
Waajiri
nchini wametakiwa kufanya uhakiki wa kina wa vyeti vya elimu kwa ajira mpya
zitakazotolewa ili kuwa na watumishi wa umma wenye sifa zinazostahili katika
utumishi wa umma.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Angellah J. Kairuki (Mb) amesema hayo leo katika kikao kazi na Watumishi wa
Umma wa Halmashauri ya Manispaa ya
Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Mhe.
Kairuki amesema uhakiki wa kina utasaidia sana kuepukana na kutojirudia tena kwa
suala la watumishi wa umma wanaoghushi vyeti.
“Jana tumetoa vibali vya ajira 10,184 kwa
Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala za Serikali, pamoja
na Taasisi na Mashirika ya Umma ili kujaza nafasi zilizoachwa na watumishi wa
umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, hivyo napenda niwasisitize sana waajiri
wote kufanya uhakiki wa kina ili tusiwe tena na watumishi wa umma wasiostahili
katika orodha ya malipo” Mhe. Kairuki amesema.
Waziri
Kairuki amesisitiza kuwa zoezi la uhakiki ni endelevu ambapo lazima lifanyika
pale mtumishi wa umma atakaporudi katika kituo cha kazi kutoka masomoni, na watakaorejea
katika utumishi wa umma baada ya likizo
bila malipo au sababu nyingine.
“Tunafanya
hivi sio kwa nia mbaya, bali tunataka tuwe na watumishi wanaostahili kuwepo
katika utumishi wa umma kwa sababu wanaoghushi wanaziba nafasi za wale
wanaostahili kuwepo na wenye sifa katika utumishi wa umma” Mhe. Kairuki
aliongeza
Pia
amewataka Waajiri kusafisha taarifa wa watumishi wa umma mara kwa mara katika
Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS).
“Kuna
watumishi ambao muda wao wa kuwepo kazini umemalizika (wamestaafu) lakini bado
wanaendelea kuwepo, Mfumo wa HCMIS sasa kila ifikapo saa 06:01 usiku utakuwa unawaondoa
wale wote ambao muda wao wa kuwepo kazini umefika lakini bado wanaendelea
kuwepo kwenye Mfumo.
Mhe,
Kairuki yuko katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Dar es Salaam, ambapo leo ni
siku yake ya nne aliyoitumia kukutana na Watendaji na watumishi wa umma wa Halmashauri
ya Manispaa ya Kinondoni, baada ya
kuzungumza na watumishi wa umma wa Temeke na Mbagala.
Lengo
la ziara ni kukutana na watumishi wa umma na kusikiliza malalamiko, ushauri na
changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili kuweza kuzifanyia kazi
na kuleta mabadiliko katika Utumishi wa Umma nchini.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi
ya Rais-UTUMISHI






0 Comments