Random Posts

Mafunzo ya Wataalam wa Dawa Afrika Mashariki yafanyika MUHAS, Dar es Salaam

 Washiriki wakiwa katika mafunzo hayo
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania, Bw. Hiiti Sillo akitoa maelezo ya utangulizi kwa washiriki
 Mgeni Rasmi, Katibu  Mkuu wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto , Dkt. Ulisubisya  Mpoki akisisitiza jambo katika hotuba yake ya ufunguzi
Picha ya pamoja baina ya Mgeni Rasmi, Katibu  Mkuu wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto , Dkt. Ulisubisya  Mpoki (wa tatu kushoto, msitari wa mbele), akiwa na waratibu, na washiriki wa mafunzo  ya kutathimini kwa ulinganifu ufanisi na usalama wa  dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Shirika la Afya Duniani (WHO) na Sekeretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wameshiriki katika uratibu wa mafunzo hayo na kutoa misaada ya hali na mali. 
..........
CHUO  Kikuu cha Tiba na Sayansi  Shirikishi  Muhimbili  kupitia Shule ya Famasi,  kwa kushirikiana  kwa Kituo cha cha Mafunzo ya Kutathimini Dawa cha Afrika Mashariki wameendesha mafunzo  ya kutathimini kwa ulinganifu ufanisi na usalama wa  dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Shirika la Afya Duniani (WHO) na Sekeretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wameshiriki katika uratibu wa mafunzo hayo na kutoa misaada ya hali na mal.i
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mgeni Rasmi,  Katibu  Mkuu wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto , Dk. Ulisubisya  Mpoki amesema mfumo kutathimini dawa za Afrika Mashariki ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wananchi wa ukanda huo wanapata dawa bora, salama na  zenye ufanisi mkubwa.

Dk. Mpoki amesema mafunzo hayo ya nadharia na vitendo kwa wataalam wa dawa wa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki yanalenga  kuhakikisha kuwa dawa zote zilizokidhi vigezo zinasajiliwa kwa mfumo wa ulinganifu unaotumika  baada wataalam hao kujiridhisha kisayansi.

Nae Mkuruenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Bw. Hiiti Sillo amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano wa karibu na wananchi katika utoaji wa taarifa pale wanapoona kuna dawa zenye mashaka ziko mtaani, hivyo kusaidia katika dhima ya kulinda afya ya jamii.

Amesema kuwa kuanzishwa kituo cha kutathimini Dawa cha Afrika Mashariki kitakuwa ni msaada mkubwa katika kuhakikisha kuwa kila dawa zilizo katika nchi za Afrika Mashariki ni zilizosajiliwa na usajili kwa matumizi ya wananchi wote wa ukanda husika.

Post a Comment

0 Comments